Thursday, April 25, 2013

MTU MMOJA ADAIWA KUFA MAJI COCO BEACH MCHANA HUU


Mwili wa marehemu ukiwa umefunikwa Khanga na wasamaria wema katika fukwe za Coco Beach....
 
Taarifa  zilizotufikia  hivi  punde  zinadai  kuwa  mtu  mmoja  (Pichani)  ambaye  bado  hajafahamika  mara  moja  amekutwa  amekufa  maji  Coco-Beach......

Tunaendelea  kufuatilia   undani  wa  habari hii......
Imetolewa  na Thimothy Shao Koko

Nakaya "Moja kati vitu ninavyojutia ni kurudisha kadi ya Chadema na kuingia CCM"

Nakaaya leo hii alikuwa kwenye interview ndani ya XXL, katika mengi aliyoyaongea, moja ni kuhusu kurudisha kadi ya Chadema na kuhamia CCM.

"moja kati vitu  ninavyojutia ni kurudisha kadi ya Chadema na kuingia CCM, najua nimebugi, lakini sio kama watu wanavyoongea kuwa nilipewa hela, kama nilipewa hela si saa hii ningekuwa nakula bata, lakini wapi! mi sijapewa hela.wanajuaje je kama nilitishiwa au vitu vingine kama hivyo..najua hapo nilibugi.Niliingia kwenye siasa kwasababu ya ushawishi wa watu, na nilishawishika kwasababu ya wimbo nilioutoa wakati hui "Mr Politician" lakini baada ya kuingia, niliona kabisa this is not what i can do, siasa ni mchezo mchafu na niliona vinani confuse" amesema Nakaaya

Wednesday, April 24, 2013

Baada ya Mama yake Zitto Kabwe Kuvamiwa na Majambazi Zitto Asema Haya

Nimekuwa naulizwa kuhusu Habari za mama yangu Mzazi Bi. Shida kuvamiwa na kutishiwa bastola. Nawajibu watu Kwa ujumla kwamba

"Moja, mie sio msemaji wa familia. Ni basi tu katika watoto wa mama yetu mie najulikana zaidi na hivyo mama anaitwa Mama Zitto. Kwetu Kigoma haitwi hivyo, ama Ni mama Salum au mama Lulu.

Pili, hili Ni suala la polisi. Lipo polisi na linashughulikiwa na polisi. Nisingependa kulisemea wakati Ni suala linalochunguzwa na polisi. Mama yangu Ni mama wa kawaida wa kitanzania kama mama mwingine yeyote yule. Matukio ya namna hii yamezagaa nchi nzima. Hivyo suala lake litashughulikiwa kama yanavyoshughulikiwa masuala mengine yote ya Watanzania. Polisi wakimaliza uchunguzi wao naamini hatua mwafaka zitachukuliwa.

Ushauri- tuwe makini na "Agente provocatuers" au in English "provocation agents" nyakati kama hizi. Calmness is the best protection against provocations. Nadhani mmenipata"

Nawatakia Kila la kheri katika kazi za ujenzi wa Taifa letu na kuimarisha Umoja na mshikamano wa Watanzania dhidi ya ufisadi, umasikini na ugandamizaji.

GODBLESS LEMA ANASAKWA NA POLISI KWA NGUVU ZOTE....WANADAI KUWA YEYE NDO MWANZILISHI WA VURUGU ZA ARUSHA LEO

 
 Kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Arusha kililazimika kutumia Mabomu ya Machozi kuwatuliza wanafunzi waliokuwa wakishinikiza kuandamana baada ya mwanafunzi mwenzao kuuawa kwa kuchomwa kisu na watu wasiojulikana majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo.  

 Tukio hilo liliamsha hisia za wanafunzi hao na kuwafanya wakusanyike kuelekea kwa mkuu wa mkoa wa Arusha kwa madai kwamba matatizo yao huwa hayafikishwi ipasavyo, hivyo wanataka kuyawasilisha wenyewe.   

Juhudi za uongozi wa chuo kuwatuliza wanafunzi hao zilishindikana, na ilipofika majira ya saa nne asubuhi, Mbunge wa jimbo la Arusha alifika katika eneo hilo kuwasikiliza wanafunzi hao. 

"Tunatoa dakika thelathini mkuu wa mkoa awe ameshafika hapa, kama hajafika ndani ya muda huo, tunaandamana wote, mimi mbele nyie nyuma mpaka ofisini kwake" alisema 

Mheshimiwa Lema.Baada ya mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio aligoma kuzungumza na wanafunzi hao, akidai kwamba hawezi kuongea mpaka Mh.Lema aondoke, ndipo atapanda kuzungumza na pia alilalamika kwamba hamna kipaza sauti kwa hiyo hawez kupaza sauti yake kuzungumza na watu wasio na nidhamu. 
 
Maneno hayo yalipandisha hasira ya wanafunzi hao lakini walitulizwa, na kipaza sauti kikaandaliwa katika ukumbi wa chuo maaruf kama "main cafetaria" ili mkuu huyo azungumze.
Wanafunzi walikusanyika eneo hilo kumsikiliza lakini alivyoanza kuongea, wanafunzi walisikika wakimzomea kwa madai kwamba ameonesha dharau.  
Wanafunzi walianza kuzomea na kumrushia chupa zaa maji na mawe  mkuu wa mkoa na hapo ndipo ilibidi mabomu ya machozi yatumike kuwatuliza wanafunzi wa chuo hicho. 
Kwa muda wa masaa mawili imekuwa ikisikika milio ya mabomu chuoni hapo mpaka hali ilipo tulia kabisa. 
Kwa sasa hali ni shwari chuoni hapo ila polisi wametapakaa huku na kule wakisema wanamtafuta Mbunge wa jimbo la Arusha kwa madai kuwa ndiye anaye chochea mgomo huo wa wanafunzi. 

Mbunge huyo alikimbia kuelekea kusikojulikana na kutelekeza gari yake chuoni hapo, ambayo polisi walilazimika kuivuta kwa "breakdown" car kuelekea kituo cha polisi. kama inavyoonekana katika picha.
Gari ya Mh.Godbless Lema ikiochukuliwa na polisi kutoka eneo la tukio
Polisi wakichukua gari ya mbunge wa jimbo la Arusha

PICHA: HUU NDO UNYAMA WALIOTENDEWA WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

Picha  ya  marehemu  Henry Koga  baada  ya  kuchomwa  kisu  na  kufariki  hapo hapo  jana  usiku  katika  chuo  cha  uhasibu  Arusha.....

Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel. 
                        Marehemu  Henry  katika enzi za uhai wake....

Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....
 
Majibu Ya Wanafunzi Hao Hayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....

Mauaji  hayo  yamesababisha  vurugu  kubwa  chuoni  hapo  zilizopelekea  kupigwa  mawe  mkuu wa  mkoa

Tuesday, April 23, 2013

Ubalozi wa Ufaransa Libya washambuliwa


Bomu limelipuka nje ya ubalozi wa Ufaransa katika mji mkuu wa Libya, Tripoli na kuwajeruhi walinzi wawili huku ikisababisha uharibifu mkubwa.

Mlipuko huo ulisababisha uharibifu katika sehemu moja ya ofisi hizo na pia kuharibu nyumba jirani.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli, Rana Jawad anasema kuwa inaaminika kuwa mlipuko huo ulisababishwa na gari lililokuwa na mabomu.

Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliitaka serikali ya Libya kuchukua hatua za haraka kukabiliana na waliosababisha shambulio hilo.
Aliongeza kwamba shambulizi hilo lililenga nchi za kigeni zinazopambana dhidi ya ugaidi.
Balozi za kigeni nchini Libya zimewahi kushambuliwa katika siku za nyuma, lakini hili ndilo shambulizi la kwanza kubwa dhidi ya ubalozi wa kigeni mjini Tripoli.
Shambulizi liliwahi kufanywa dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi mwezi Septemba mwaka jana na kusababisha kifo cha balozi Christopher Stevens pamoja na maafisa wengine wamarekani .
Shambulio la leo lilifanyika muda mfupi baada ya saa kumi na moja asubuhi katika mtaa wa kifarahari mjini Tripoli.
Wakaazi wa eneo hilo walighadhabishwa sana na shambulizi hilo na kulalamikia ukosefu wa ulinzi mzuri wa sehemu hiyo.
Waziri wa mambo ya nje wa Libya, Mohammed Abdel Aziz alilaani vikali shambulizi hilo, ingawa hawajaeleza ni nani wanayemshuku kulifanya.
Chanzo:BBC SWAHILI

PADRI ADAIWA KUMKATA MAPANGA MWANAMKE ALIYEZAA NAE


Vitendo vya kikatili vimekuwa vikitekelezwa katika sura mbalimbali, ila tukio la mtumishi wa Mungu, Padri Celestine John Nyaumba, 35, kumgonga kwa gari makusudi na kumcharanga mapanga mzazi mwenzake ni aibu isiyo na mfano.
Padri Celestine, anayetoa huduma kwenye Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, Homboro, Dodoma, anatuhumiwa kumtendea unyama huo, mzazi mwenzake, Selestina Anania Kibena, 35, Jumamosi iliyopita, Kata ya Kiluvya, Pwani.
Hii ni aibu isiyomithilika kwa sababu padri kufanya ukatili huo ni kashfa nzito, ongezea kwamba alimfanyia hivyo mzazi mwenzake, wakati kwa sheria za kanisa, ni mwiko kwa padri kujihusisha na mapenzi achilia mbali kufikia hatua ya kuzaa.
Aibu hiyo, inapata uzito zaidi kwa kuwa Selestina (mzazi mwenza wa padri), alikuwa mtawa (sister), lakini usista ulimshinda baada ya kupata mimba, takriban miaka minne iliyopita.

TUKIO LILIVYOKUWA
Padri Celestine, akiwa anaendelea na utoaji wa huduma kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph, alipata nafasi ya kujiendeleza kimasomo, Chuo Kikuu cha Ardhi, Kitivo cha Ubunifu na Uchoraji wa Majengo, Dar es Salaam.
Akiwa Dar, Padri Celestine anaishi Mbezi Shamba, wakati Selestina ni mkazi wa Maili Mbili, Dodoma.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, mapema wiki iliyopita, Padri Celestine, alimwita Selestina, aungane naye Dar es Salaam, ‘wapumzishane’ kwa siku chache, kwani inadaiwa kwamba uhusiano wao wa kimapenzi ulikuwa unaendelea kwa siri.

MPANGO WA KIKATILI
Habari zinatiririsha mambo kama ifuatavyo:
Ijumaa iliyopita, Selestina aliwasili Dar es Salaam na kufikia nyumbani kwa Padri Celestine.
Siku hiyo (Ijumaa), walizungumza mengi, ikiwemo kupanga mambo mbalimbali kuhusu maisha yao na mtoto wao ambaye sasa ana umri wa miaka mitatu.
Siku iliyofuata (Jumamosi iliyopita), Padri Celestine, alimwomba Selestina, waongozane kwenda Kiluvya, Pwani.
Selestina hakuwa na shaka juu ya hilo lakini akataka sababu ya kwenda Kiluvya, badala ya sehemu nyingine.
Celestine akamweleza kuwa Kiluvya kuna sehemu nzuri ya kupumzika, vilevile ana jambo la kikazi atalifanya akiwa huko.

UKATILI UKATENDEKA
Ilipofika usiku wa siku hiyo (Jumamosi), Padri Celestine na Selestina, walianza safari ya kutokea Mbezi Shamba kwenda Kiluvya, wakiwa na gari aina ya Suzuki lenye namba za usajili T220 AJN.
“Walipofika Kiluvya, Padri Celestine ambaye alikuwa anaendesha gari hilo, alikata kushoto kuelekea porini. Gari likiwa porini kabisa, Padri Celestine alisimamisha kisha akamwambia Selestina ashuke kuangalia chini, kwani alihisi kuna tatizo,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Selestina alishuka akainama chini kwenye uvungu wa gari kuangalia tatizo, ile anafanya hivyo tu, Padri Celestine aliendesha gari kwa spidi ili amgonge Selestina. Bahati nzuri Selestina aliruka lakini gari lilimgonga kwenye paja la kushoto.
“Baada ya hapo, Celestine aligeuza gari amgonge tena lakini Selestina alijirusha sehemu yenye kishimo fulani hivi, kwa hiyo gari lilikuwa haliwezi kumfikia. Kuona hivyo, Padri Celestine alianza kumpiga mawe Celestine.
“Pengine aliona yale mawe hayana uzito wa kutimiza kile ambacho alitaka kukifanya kwa Selestina, kwa hiyo Padri Celestine alifuata panga kwenye gari, akamfuata Selestina, akamcharanga mapanga kichwani, kwenye mikono yote miwili na mguu wa kushoto.
“Kabla hajaendelea zaidi, Selestina alimrukia, purukushani ikaendelea. Padri Celestine alimng’ata Selestina katika shavu la kushoto, mwanamke huyo naye akajibu mapigo, akamng’ata padri katika shavu la kulia.
“Baada ya purukushani ya muda mrefu, Padri Celestine aliona mambo magumu, ikabidi amwombe msamaha Selestina kwamba shetani alimpitia, akamwomba ampeleke hospitali.
“Selestina alikubali lakini ile Padri Celestine anafuata gari, Selestina alijitutumua na kukimbia mbali zaidi, Padri Celestine aliporudi pale alipomwacha, hakumwona tena.”

HOSPITALI NA POLISI TUMBI
Chanzo chetu kilisema: “Selestina alijivuta mpaka Hospitali ya Mkoa wa Pwani, Tumbi. Vilevile alitoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Tumbi.
“Polisi walianza kufanya upelelezi wao na kufanikiwa kumkamata Padri Celestine, Jumapili iliyopita jioni.”

RPC ANENA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei, alikiri kutokea kwa tukio hilo na akafafanua kwamba baada ya Padri Celestine kuhojiwa, alisema alipitiwa na shetani kutokana na usumbufu aliokuwa anaupata kutoka kwa Selestina.
Kamanda Matei alisema, Padri Celestine alidai kuwa Selestina alikuwa anamuomba fedha nyingi za matumizi kwa ajili ya mtoto wao, kwa hiyo shetani alimpanda na kufikia hatua ya kufanya kile alichokitenda.

SELESTINA NAYE AZUNGUMZA
Akiwa amelazwa Hospitali ya Tumbi, Selestina alisema: “Nashangaa kwa kila kilichotokea. Niliitwa na Padri Celestina kuja kupumzika, nashangaa mapumziko yamegeuka mateso.”

MFANYABIASHARA WA KIHINDI ADAIWA KUMNYONGA MWALIMU DAR


Simanzi, majonzi na masikitiko makubwa yalitawala katika msiba wa Mwalimu Elizabeth Mmbaga, 22, aliyekutwa amefariki dunia chumbani kwake Kimara Baruti jijini Dar, Aprili 15 mwaka huu,

Mwalimu Elizabeth Mmbaga enzi za uhai wake
Habari kutoka eneo la tukio zinadai kuwa, kifo cha mwalimu huyo wa Shule ya Msingi Atlas ya jijini Dar kimezua utata kutokana na jinsi mwili wake ulivyokutwa na kusababisha minong’ono ya kwamba amenyongwa na mfanyabiashara mmoja wa Kihindi (jina halikuweza kupatikana mara moja) ambaye alikuwa mpenzi wake.

Baadhi ya wazazi wa shule aliyo kuwa akifundisha marehemu, wakiaga mwili
UWAZI KAZINI
Uchunguzi wa gazeti hili umeonyesha kuwa, Aprili 14, mwaka huu Jumapili usiku, Mhindi mmoja alionekana akiwa na Elizabeth maeneo ya jirani na nyumbani kwa marehemu.
“Siku hiyo tulimuona marehemu akiwa na yule Mhindi baa wakinywa vinywaji karibu kabisa na alipokuwa akiishi Eliza na ilipofika usiku, wawili hao  waliondoka pamoja.
“Kesho yake ndiyo tukasikia Eliza amekutwa akiwa amekufa chumbani kwake, kimsingi kama yule Mhindi atapatikana anaweza kuisaidia polisi kwani inavyoonekana anahusika na kifo hicho,” kilidai chanzo hicho kinachoishi jirani na marehemu.
Baadhi ya wanafunzi wakilia kwa uchungu
UGOMVI WA KIMAPENZI WATAJWA
Mmoja wa marafiki wa marehemu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema kuwa, mara kwa mara amekuwa akiwasuluhisha Eliza na mpenzi wake huyo chanzo kikiwa ni mambo ya mapenzi na kwamba hakujua kama ugomvi huo ungeishia kwenye kifo.
“Kwa kweli inasikitisha, Eliza na yule mpenzi wake walikuwa wakigombana sana, chanzo ni haya haya mambo ya mapenzi. Nilidhani ni kutofautiana kwa kawaida tu lakini sikujua mwisho utakuwa mbaya,” alisema rafiki huyo wa marehemu.
Akazidi kudai kuwa, Mhindi huyo ambaye ni mfanyabiashara alikuwa akitaka kumuoa Eliza lakini tatizo likawa tofauti za kidini ambapo mwanaume huyo aliumia kumkosa na ikadaiwa huenda ndiyo chanzo cha mauaji hayo.
Chanzo kingine kikadai kuwa, Mhindi huyo siku chache kabla ya tukio alimdanganya Eliza kwamba muda wake wa kuishi hapa nchini umeisha hivyo kumtaka waonane ili waagane na amuachie fedha za matumizi.
“Inavyoonekana marehemu alimuamini Mhindi huyo na kuamua kwenda kuonana naye bila kujua kuwa ndiyo ilikuwa siku ya mwisho ya uhai wake.
“Mbaya zaidi baada ya Eliza kukutwa amekufa, pembeni zilikutwa simu zake tatu ambapo moja ilikuwa na ujumbe unaoonesha ulitoka kwa jamaa huyo akisema ametimiza alichotaka na ameondoka zake.”

HALI ILIVYOKUWA CHUMBANI
Mwili wa mwalimu huyo aliyekuwa maarufu kwa jina la Ticha Eliza ulikutwa na walimu wenzake waliokwenda kumwangalia nyumbani kwake ukiwa chumbani juu ya kitanda huku chaga zikiwa zimevunjika.
“Tulilazimika kwenda nyumbani kwake baada ya kumpigia simu na ikawa inaita bila kupokelewa,” alisema mmoja wa walimu hao aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini na kuongeza:
“Ndani ya chumba tulikuta vitu vimevurugika huku mwili wa marehemu ukionekana kuwa na alama shingoni na kwamba vitu vilivyokuwa chumbani humo vilikuwa vimevurugika, hali iliyoashiria kulikua na ugomvi au nguvu kubwa kutumika wakati wa mauaji.”

BOSI WA ELIZA ANASEMAJE?
Mwalimu Mkuu, Moses Kyambo wa shule ya Atlas akizungumza na Uwazi kuhusiana na kifo hicho alisema wameshituka sana kwani kimetokea ghafla na marehemu alikuwa haumwi.
“Siku hiyo ya Jumatatu marehemu hakuonekana shuleni asubuhi jambo ambalo siyo kawaida yake kwani hakutoa taarifa ya kutofika, mazingira hayo yalimfanya mwalimu wa taaluma Donard Otiato kumpigia simu ambazo zilikuwa zinaita bila kupokelewa.
“Ilipofika jioni baadhi ya walimu wenzake walilazimika kwenda nyumbani kwake Kimara Baruti na walipofika waligonga mlango bila kuitikiwa, mmoja wao aliusukuma wakaingia ndani na kumkuta amelala kitandani.
“Walimuita lakini hakuitika, walipomuangalia vizuri waligundua kuwa amefariki dunia huku damu zikimtoka mdomoni, puani na ulimi ulikuwa umetoka nje. Pia alikuwa na alama za michubuko shingoni na sehemu nyingine za mwili huku vyombo vya ndani vikiwa vimevurugika.
“Ilivyoonekana kulikuwa na mapambano kati ya marehemu na muuaji. Walimu hao walinipigia simu na kunifahamisha walichokikuta, nikawaelekeza waite polisi au watoe taarifa.
 “Nilitoka kuelekea eneo la tukio, nikawakuta polisi wameshafika na walikuwa wanaendelea kuchukua maelezo kwa baadhi ya wananchi wa eneo hilo.
 “Kwa kweli tumempoteza mtu muhimu sana kwa shule yetu kwani marehemu alikuwa ni mchapakazi na mwenye ushirikiano mzuri kwa wenzake,” alisema mwalimu huyo.

WALIMU, WANAFUNZI WAZIMIA
Mwili wa Elizabeth uliagwa kwenye Shule ya Atlas huko Madale, Wilaya ya Kinondoni Jumatano ya wiki iliyopita na ukasafirishwa kupelekwa Karatu mkoani Arusha kwa mazishi.
Kilichoongeza simanzi ni wakati wa zoezi la kuuaga mwili wa marehemu ambapo baadhi ya walimu na wanafunzi wa shule hiyo walilia hadi kufikia hatua ya kuzimia.
Aidha, kiongozi wa dini aliyekuwa akiendesha ibada ya mazishi aliyefahamika kwa jina la Mchungaji Leonard alisema muuaji wa mwalimu huyo atahukumiwa na Mungu kwani alichokifanya ni kitu kibaya sana.

RPC KENYELA ANENA
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kinyela amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kwamba uchunguzi unaendelea.
 “Ni kweli nina taarifa juu ya tukio hilo na tunaendelea kufanya upelelezi ili kubaini chanzo, tutakapopata taarifa za daktari na kuthibitisha kuwa alinyongwa, tutaanza kazi ya kumtafuta mhusika,” alisema Kenyela.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI WA MADHEHEBU MBALIMBALI YA DINI YA KIKRISTO LEO IKULU‏

Juu na chini anaonekana Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kikristo Ikulu jijini Dar es salaam leo ambapo amekuwa na mazungumzo nao ikiwa ni mojawapo ya jitihada za Rais
Kikwete kutafuta muafaka na kutafuta utatuzi wa hali ya sintofahamu ambayo
inanyemelea nchi yetu katika kipindi hiki.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kikristo Ikulu jijini Dar es salaam leo
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini ya Kikristo Ikulu jijini Dar es salaam leo. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano) Mhe Steven Wassira.
----
Viongozi wa dini wamewataka waumini
kote nchini kulinda amani na  umoja uliopo
 ili nchi isije ikaingia kwenye
mgawanyiko wa kidini na kuleta machafuko hapa Tanzania.

Wito huo umetolewa na viongozi wa dini
leo Ikulu ya Dar-Es-Salaam mara baada ya kikao cha pamoja baina ya viongozi wa
dini na Rais Jakaya Kikwete.
Viongozi hao wa dini wamefika leo
wakiongozwa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza
la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Viongozi wengine wametokea Baraza la Kikristo
Tanzania (CCT) Seventh Day Advertist (SDA) na Baraza la Pentekoste Tanzania (PCT).

Mkutano huo umeanza kwa Askofu
Ngalalekumtwa kusoma tamko lao la pamoja kwa Rais Kikwete ambalo ndilo limetoa
muongozo wa mazungumzo hayo ya leo ambayo yamehusu Amani na Usalama wa Taifa na
migogoro ya kidini ndani ya jamii.

Mkutano wa viongozi wa dini ya
Kikristo Tanzania ni mojawapo ya jitihada za Rais Kikwete kutafuta muafaka na
kutafuta utatuzi wa hali ya sintofahamu ambayo inanyemelea nchi yetu katika
kipindi hiki.

“Nataka tuzungumze ni namna gani
tunaweza kutoka kwenye hali hii na tunakwendaje mbele zaidi na kuhakikisha nchi
yetu bado inakua ya  amani na umoja kama
ilivyozoeleka”
Rais amesema na kutoa nafasi kwa viongozi wa dini kutoa maoni yao.

Viongozi hao wa dini wamemueleza Rais
Kikwete kuwa wanaunga mkono jitihada zake za kutafuta amani na kwa pamoja
wamekubaliana uandaliwe mkutano wa pamoja baina ya viongozi wa dini zote ambapo
masuala ya amani na umoja wa nchi utajadiliwa kwa kirefu.
Katika kikao cha leo pande zote
zimekubaliana kuwa kuna changamoto zilizoko sasa zinahitaji kutatuliwa haraka
iwezekanavyo ili kuepusha nchi kutumbukia katika mgogoro mkubwa zaidi, na pia
kukubaliana kuwa pande zote, kwa maana ya serikali na taasisi za dini,
zinawajibu mkubwa wa kuhakikisha amani inadumu.
Kabla ya kikao cha leo , Rais amewahi
kukutana na viongozi wa dini ya kiislamu na kikristo mmoja mmoja ambapo alikua
akitafuta maoni na ushauri wa pande zote kabla ya pande zote hazijakaa pamoja
na kuwa na msimamo wa pamoja.

Kikao cha leo kimehitimisha jitihada
hizo na kinachofuata ni mkutano mmoja ambapo Rais Kikwete atakutana na viongozi
wa dini zote kwa pamoja hivi karibuni.
………...”MWISHO”……..

Imetolewa na:

Premi
Kibanga,

Mwandishi
wa Habari wa Rais, Msaidizi,

Ikulu-DSM

23
Aprili, 2013

Tundu Lissu "Matusi Yataisha Bungeni Endapo Spika Ataacha Upendeleo"

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, amesema fujo zitaisha bungeni ikiwa Spika wa Bunge, Naibu na Wenyeviti watafuata na kusimamia kanuni za Bunge bila kupendelea upande wowote.

Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, aliyasema jijini Dar es Salaam jana wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha ITV.

Alisema fujo hazitaisha kama watu hawatafuata kanuni na Spika kusimamia na kuzingatia mamlaka yake bila ya upendeleo wowote.
“Tatizo kubwa Spika anafanya kazi bila kufuata kanuni za Bunge. Kuna mambo mengine anayatolea maamuzi bila kufuata kanuni za Bunge. Mfano suala letu la adhabu tuliyopewa wabunge watano wa Chadema ya kutohudhuria vikao vitano. Hakuna katika kanuni za Bunge.
Spika alipaswa kupeleka majina yetu katika Kamati ya Maadili ili ichunguze na kupendekeza adhabu kisha ipeleke taarifa bungeni na Bunge ndilo litoe adhabu," alisema.

Alisema kama utaratibu ndani ya Bunge unakiukwa, Chadema wataendelea kupinga hata kama watafukuzwa kila mara kwani wasipofanya hivyo athari yake itakuwa kubwa hapo baadaye.

“Hata kama watu wote watasema niache kuongea, nasema siwezi kuacha mimi ni mbunge na sehemu yangu kubwa ya kazi ni bungeni. Hivyo nikifika huko lazima nitazungumza, kama sitazungumza ndani ya Bunge, nitazungumza nje na nikirudi tena ndani nitalizungumza,” alisema.

Lissu aliongeza kuwa hulka ya Bunge ni kelele na hii si hapa nchini tu, bali hata nchi nyingine, ila tatizo la Watanzania ni uchanga wa mfumo wa vyama vingi na ndiyo maana wanaona mambo hayo kama ni mageni.
CHANZO: ALASIRI

Lady Jay Dee Ampa 5 Ben Pol ... Ni Baada Ya Kumuimba Kwenye Track Yake Mpya

Hata baada ya yale tuliyoyaona kabla ... Mwanadada anaetamba na wimbo wake wa JOTO, HASIRA ... LADY JAYDEE amempongeza na kumpa 5 mwanamuziki mwenzie ... BEN POL ...

Lady JayDee ambae few minutes ago, ametweet, "Wooh!! @IamBenPol So nimeskia umeimba unampenda Lady Jaydee !! Kula 5 kwanza mengine yatafuata baadae " ...

Ben Pol nae akajibu, "Yeeaaah!! nakupa then inakuwa #Celebratiiiooons" ...

Lady Jaydee na Ben Pol waliwahi kukwaruzana kupitia mtandao huo wa twitter na kuwa katika hali ya kutoelewana kabisa ...

Katika ngoma mpya ya Ben Pol ambayo anatarajia kuitoa mwisho wa mwezi huu, ame-release TEASER yake inayofahamika kama #JIKUBALI na amemtaja Lady Jaydee katika mwanzo wa wimbo huo ...

Katika mazungumzo yao mtandaoni, Lady Jaydee alimaaliza kwa kutweet, "Good boy " ...

Well, this is more of LETS BURY THE HATCHET ... This is very good hasa kwa wasanii kama hawa wanaofanya vizuri na kufaa kuigwa ...

Monday, April 22, 2013

TUNAUZA MAFUTA YA ALIZETI KWA BEI YA JUMLA

 

JIPATIE MAFUTA YA ALIZETI KUTOKA DODOMA KWA BEI NAFUU
SHILINGI 55,000 KWA LITA 20 NA 15,000 KWA LITRE  5
PIA NA MAFUTA YA UBUYU YANAPATIKANA KWA BEI YA JUMLA NA REJAREJA
FOR SERIOUS BUYER CONTACT
0717998931 or 0714547598 


BABY MADAHA: NTAWACHANGANYA WANAUME KAMA DIAMOND


STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ amesema mwaka huu atawachanganya wanaume kama afanyavyo Nasibu Abdul ‘Diamond’ ili kwenda sawa.
Akifafanua kauli yake kwa paparazi wa Stori 3, Baby Madaha aliweka bayana kuwa haoni tatizo kunaswa na Mwisho Mwampamba kama ilivyoripotiwa hivi karibuni wakati huohuo anatoka kisela na mkali wa Bongo Fleva, Juma Kassim ‘Nature’.
“Watakoma mwaka huu, lazima niwachanganye sana, mbona wao wanatuchanganya sana kama Diamond vile anavyofanya!” alisema Baby.

Mahakama ya rufaa yatupilia mbali Rufaa ya Kupinga ushindi dhidi ya Lema!!



Ombi la kwanza la waleta rufani la kutaka review ya uamuzi uliotolewa na mahakama ya rufaa juu ya kesi ya Mh.Lema na kutaka isikilizwe na jopo la majaji 7 limetupiliwa mbali leo katika mahakama ya rufaa na sasa ni majaji walewale waliotoa hukumu wanapitia.Mahakama imetupilia mbali madai ya kwanza kwa kuwa hayapo based on merits


Kesi hii ilifunguliwa tena baada ya Mh.Lema kushinda rufaa tarehe 21 desemba 2012,kesi iliyosimamiwa na mawakili maarufu sana baada ya kuzungushwa kwa muda mrefu.Warufani safari hii wanataka mahakama ipitie upya uamuzi uliotolewa na jopo la majaji watatu na wametaka benchi la majaji saba.


Mahakama imetupilia mbali mashtaka yao na mahakama imewaamuru tena wakata rufaa walipe gharama zote za kesi.

Wafuasi wa CHADEMA wanashangilia sana muda huu eneo la mahakama

Wakenya Wasema "Mr.Nice anafaa kuheshimiwa, anakipaji special ambacho kinafaa kutunzwa"

Siku chache baada ya record lebel ya Grand Pa ya Kenya kutangaza kumsaini Mr. Nice, DNA ambae pia ni member wa lebel hiyo amefunguka kuhusu jinsi walivyompokea member huyo mpya katika familia ya Grand Pa.

Akizungumza na Milazo 101 ya Radio One amesema Mr. Nice anafaa kuheshimiwa kutokana na uwezo wake na kwamba ana kipaji special ambacho kinafaa kutunzwa. Amefafanua kuwa wao ndio waliomtafuta mwanamuziki huyo ambae wanaamini bado anapendwa sana na fans wake hususani nchini Kenya.

“Mr. Nice hakuomba nafasi tulimtafuta sisi, kwa sababu tunatambua kipaji chake na tunajua kwamba wasanii sio kama karatasi ya choo, sio kama mtu akinyamaza amepotea na tena hana kazi. May be unakuta labda hako na management ama kuna issue flani ya kibinafsi mtu akanyamaza. Mr. Nice ndiyo kabisa kutoka Tanzania ianze yeye ndiye alifanya bongo ikajulikana Afrika mashariki na anafaa apewe nafasi tena na tena na tena.”

Alifunguka zaidi kuwa Grand Pa kwa kushirikiana na Mr. Nice wanaweza kumrudisha Yule Mr. Nice wa kipindi kile.

“Grand Pa kwa kushirikiana na Nice anaweza akarudi, Grand Pa yenyewe haiwezi. Nice mwenyewe alifanya nyimbo ambazo sasa hivi bado zinagongwa Kenya baada ya miaka nane miaka kumi unajua, it means jamaa bado ako na kipaji special ambacho kinafaa kutunzwa. Wasanii wengi wanavipaji lakini wanakosa kufaulu because hawana Management, ndo hivyo sasa Mr. Nice yuko ndani ya Nyumba tunafanya nae.”

Hata hivyo uongozi wa Grand Pa umemzuia kwa muda Mr. Nice kuzungumza na Media kwa sababu za kiutawala hadi pale watakapoanza tour yake nchini Kenya hivi karibuni.

LADY JAYDEE: MNAFIKI WA MIAKA 10, SHUJAA WA SIKU 30

Imeandikwa na Saleh Ally via wavuti.com

MGOGORO wa kimuziki kati ya msanii Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ na kituo kimoja cha redio umezidi kuchukua kasi huku makundi mawili, kila moja likitengeneza ngome yake na kuamini linachoamini.

Kundi ambalo linamuunga mkono Jaydee na kumuona ni mkombozi, anazungumza kwa niaba yake na wasanii wengine, la pili ni lile linalobaki upande unaoshambuliwa, linatetea ngome yake.

Jaydee anashutumu kubaniwa nyimbo zake na kituo hicho ambacho kupitia mitandao kadhaa ya kijamii ameeleza wazi kuwa wanambania, wanaziponda lakini hata watangazaji wake wamekuwa wakionyesha chuki binafsi dhidi yake.

Jaydee pia aliwaponda wasanii Ben Pol na Linah anayetokea THT kwamba walishindwa kutokea kwenye uzinduzi wa video ya wimbo wake wa Joto Hasira, kwa madai walizuiwa na bosi wao.


Ujasiri huu wa Jaydee ndiyo kitu bora ambacho kimekuwa kikitakiwa kufanyika kutoka kwa wasanii, yaani wapigane kutetea muziki wa Tanzania hasa kama kuna watu au kundi la watu limejikita katika kuuangamiza.

Lakini ni tofauti kidogo, kwani wasanii wengi wamekuwa imara na kuwa tayari kujitetea wenyewe tu na si vingine. Nasisitiza mara nyingi, wao ndiyo wahusika wa kwanza na wanapaswa kuanzisha mapinduzi kuanzia kwao, mfano kusema naonewa si kitu kibaya lakini je, umewahi kupigania wanaoonewa?

Kujitetea pekee unaweza kufanya, lakini vipi utafanikiwa kama asilimia kubwa ya kundi la wanamuziki linaendelea kuonewa. Ukibaki hauonewi pekee na asilimia kubwa ya wasanii au wanamuziki inaonewa, kunaweza kuwa na 
mapinduzi sahihi?

Ndiyo maana nashangazwa kusikia Jaydee leo anaona ubovu wa kituo hicho, anathubutu kusema hadharani akionyesha wazi ameumia. Lakini miaka 10 au zaidi iliyopita, Jaydee alikuwa kimya na hakuwaza kusema kwamba kituo hicho kinawabania wasanii wengine na ‘kumtukuza’ yeye hata kama muziki wake haukuwa wa kiwango kilichokuwa kinazungumzwa.
Siwezi kusema muziki wa Jaydee ni mbaya, nimekuwa kati ya mashabiki wake. Lakini yoyote atanichekesha akisema nyimbo albamu zake zote alizotoa zilikuwa katika kiwango cha juu sana na ndiyo maana leo ni maarufu.

Hakuna asiyejua kwamba miaka nenda rudi, wasanii wamekuwa wanaongoza kwa unafiki, kutopendana wenyewe, kugeukana na hata kujenga makundi lukuki, ndiyo maana kila kukicha wamekuwa wakishambuliwa maana katika maisha yao hawana umoja.

Jaydee alianza kuwa mtangazaji katika kituo hicho baada ya kuacha kurap, akaamua kuachana na kurap na mwisho kuwa msanii wa nyimbo za kubembeleza, mara ya kwanza akianza kutikisa na albamu ya Machozi, Solo Thang anaweza kuhadithia vizuri kuhusu hili.

Kuanzia albamu ya Machozi, kituo hicho ndicho kilisimama kuhakikisha anakuwa bora hata kama muziki wake haukuwa ukimzidi kila mwanadada wakati huo.

 Angalia, kulikuwa wasanii kama Stara Thomas, Carola Kinasha ambao kiuwezo walikuwa juu kuliko Jaydee, lakini hawakupewa nafasi ya kutosha, badala yake Jaydee ambaye hakuthubutu kuwatetea hata kidogo akaendelea ‘kubebwa’ na watu wakaamini ni bora kuliko yeyote kwa upande wa akina dada au kina mama katika kuimba, haikuwa hivyo.

Angalia albamu ya Binti, karibu nyimbo zote zilikuwa na ujumbe mmoja, ulikuwa ukimshambulia mwanaume mmoja ambaye alikuwa amemuumiza Jaydee. Takribani ujumbe wa nyimbo karibu zote ulikuwa ni mmoja, lakini ilibebwa na kuonekana ni moja ya albamu bora kabisa kuwahi kuwepo katika muziki wa Tanzania, kitu ambacho hakikuwa sahihi.

Wakati huo wasanii lukuki walilia kubaniwa, mmoja wao alikuwa ni Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye ndiye alimtambulisha mwanadada huyo alipomshirikisha katika wimbo wa Mambo ya Fedha, kabla ya hapo hakuwa na jina. 
Jaydee hakuwahi kuungana naye hata kidogo hata kwa mstari mmoja wa kumtetea au kuunga mkono kutetea muziki wa Tanzania, kuonyesha anapinga mwenendo wa wanaolazimisha kuwabagua wasanii au kufanya mambo kwa mabavu kwa kuwa wameshika mpini.

Hakuna aliyesikia kilio cha Sugu, wasanii wanaochipukia bila ya kujua wasemacho, kisa nyimbo zao zinapigwa redioni, ili kuonyesha shukrani za dhati wakaanza kutangaza Sugu anatapatapa na amekwisha kimuziki!

Ajabu, asilimia kubwa ya maneno yake ndiyo yanayozungumzwa leo, ndiyo yanatumiwa na kila msanii anayebanwa au kuhisi kaonewa. Angalia, hata Jaydee naye ameingia huko! Swali langu hapa je, Jaydee na wengine wanaolalamika, wamekwisha kisanii?

Ndiyo maana nasema, tasnia ya muziki hasa muziki wa kizazi kipya umejaza watu wavivu kufikiri, wenye mioyo ya ‘Kichina’, wasio na uwezo wa kuthubutu hata kidogo ambao wanasubiri wayumbe au kuumizwa wao ili wamtafute wa kumuangushia lawama.

Jiulize, kama Jaydee alibebwa kwa miaka 10, halafu leo analalamika atakuwa sahihi? Sitaki kumpinga kwa kuwa kuna kitu anakiona lakini ninaamini alikiona tokea mapema, akauchuna.

Bado nasisitiza, yeye na wengine wote wanaolia baada ya kuguswa wao nawaita wanafiki, wanapigana kwa ajili yao na si kwa muziki wanaoutumikia. Iwapo wangekuwa tayari kupambana kwa ajili ya muziki huo, msanii kama Jaydee asingeanza vita leo.

NARUDI KWA JAYDEE


Sijawahi kuingia naye katika malumbano zaidi ya miaka 10 tokea alipokuwa mwanahabari mwenzangu na sasa msanii. Lakini nathubutu kumueleza kuwa ni kati ya wasanii wasiojali muziki wa Tanzania na wanajiangalia wao zaidi.

Picha ya unafiki na kujiangalia mwenyewe inaonekana sasa ingawa takribani miaka mitano iliyopita nilianza kuinusa. Leo analia, anabaniwa na anauona moto unaounguza muziki wa Tanzania ulivyo mkali.

Naamini aliuona miaka kibao nyuma, lakini kwa kuwa alikuwa akitetewa hakuweza kuangalia kwamba rafiki zake, wasanii waliombeba kabla walikuwa wakiungua. Akaendelea kuwapita kwa raha zake mustarehe.

Tungeweza kumuita Jaydee ni mpambanaji kama angewakosoa hao anawakosoa sasa katika kipindi walichokuwa wamempa mbeleko yeye, basi kweli ingeonekana anapigania muziki wa Tanzania. Sasa anapigania chake tu!

Jaydee amefika mbali kimuziki, alikuwa bora jukwaani na nyimbo kadhaa na nyingi zikapewa ‘over promotion’ lakini bado ninaweza kumuita mkongwe. Ajabu alibaki chipukizi hadi leo katika suala la kutetea haki za wasanii na muziki wenyewe.

Sitaki kumkatisha tamaa kwa mapambano aliyoyaanza, ninaamini ana nafasi ya kuanza kuusaidia muziki ambao umemsaidia. Lakini ndiyo kipindi ambacho anaweza kupata machungu waliyopata wasanii wenzake kunyeshewa mvua na kuunguzwa na jua wakati akiwa kivulini kwa ‘msaada’.

Anachokifanya leo Jaydee ni nyongeza tu ya walichokifanya Sugu au Afande Sele au wasanii wachache walioamua kuwa wakweli au wale walioamua kuwa wabunifu kama Ambwene Yessaya ‘AY’, aliyekimbia vita ya redio na kuingia katika kurekodi video bora zilizoendelea kumng’arisha.

Simzuii, Jaydee kuendelea kupambana, lakini namuasa anachokifanya kama ni kwa ajili ya muziki akipozwa tena, asirudi nyuma.

Ninachomkumbusha, hata yeye amekuwa kundi moja na analowalaumu ambao angeweza kuwashauri mapema ‘ndani ya mjengo’ kama angekuwa na nia nzuri na muziki wa kizazi kipya.  Msisitizo ‘Joto Hasira’ liwe la kweli.

PREZZO AUMBUKA BAADA YA PICHA YAKE YA UTUPU KUVUJA


Jackson Makini a.k.a. Prezzo is in trouble…..on Saturday after the release of his new and controversial track Liqher,  his n*ked photos enjoying some private time with two lasses were leaked to the internet.

Check out the first PHOTO>>>
Source:Daily post

Sunday, April 21, 2013

Wabunge wa Chadema kuweka kambi majimbo ya Makinda, Ndugai

Wabunge sita wa Chadema waliosimamishwa bungeni wameamua kwenda kuwashtaki Spika Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai kwenye majimbo yao.
Wakitangaza uamuzi huo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi ya Mbugani, Mwanza jana, walisema pia watakwenda kwenye majimbo ya wabunge wawili wa CCM, Mwigulu Nchemba (Iramba Magharibi) na Livingstone Lusinde (Mtera) ili kueleza jinsi wabunge wa upinzani wanavyokandamizwa bungeni.

Ndugai, ambaye ni Mbunge wa Kongwa (CCM), aliwasimamisha wabunge sita wa Chadema kuhudhuria vikao vitano vya Bunge kutokana na kile alichokiita kufanya vurugu bungeni. Hatua hiyo ya Ndugai aliyoichukua Aprili 17, mwaka huu ilipata baraka za Spika Makinda Ijumaa iliyopita.

Wabunge waliosimamishwa ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Godbless Lema (Arusha Mjini), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Ezekiah Wenje (Nyamagana). Katika mkutano huo ulioanza saa 9.30 alasiri na kumalizika saa 12.00 jioni, ulihudhuriwa na wabunge wanne kati ya hao. Mbilinyi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuhutubia akifuatiwa Mchungaji Msigwa, Kiwia na Wenje. Lissu na Lema hawakuhudhuria.

Akizungumzia ziara yao katika majimbo ya viongozi hao wa Bunge, Mchungaji Msigwa alisema itakuwa ya kuwashtaki kwa kuendesha Bunge kuwapendelea wabunge wa CCM hata wanapofanya makosa ya wazi.

Alidai kuwa wabunge wa CCM ndiyo vinara wa lugha chafu bungeni na kuwatolea mfano Mwigulu na Lusinde. Pia alizungumzia tusi zito lililotolewa na Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM), Peter Serukamba, Aprili 17, mwaka huu.
“Kila mtu alimshuhudia Serukamba alipoporomosha tusi zito, lakini Spika na Naibu wake hawakuchukua hatua zozote.

“Lissu na sisi wengine tumeadhibiwa kwa kosa la kuomba mwongozo wa Spika. Hapa wananchi mnaona kuna haki kweli,?” alihoji Mchungaji Msigwa huku akishangiliwa na wafuasi wa chama hicho.

Alisema watapita kwenye majimbo ya wabunge wa chama hicho waliosimamishwa ili kuwaelimisha wapigakura wao.

Alisema wataanza ziara majimboni kesho wakianzia Iramba Magharibi kumshtaki Nchemba. Baada ya hapo watakwenda Singida Mashariki kwa Lissu ili kuwapa ukweli wapigakura wake.
Mchungaji Msigwa alisema baada ya hapo watakwenda Kongwa kwa Ndugai na kisha Mtera kwa Lusinde kabla ya kuelekea Njombe Kusini kwa Makinda. Pia watakwenda Iringa, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha.

Hata hivyo, ziara ya wabunge hao kwenda mkoani Mbeya imekwaa kisiki baada ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Athumani Diwani kukataa kutoa kibali.

Kumlipua kigogo CCM
Mchungaji Msigwa ameahidi pia kulipua bomu la kigogo wa ngazi ya juu wa CCM, ambaye alidai kuwa anajihusisha na ujangili wa meno ya tembo atakaporejea bungeni baada ya kumaliza adhabu yake wiki hii.

Wenje ataja safu ya 2015
Wenje aliwaambia wafuasi wa chama chake kuwa kimejipanga kushinda Uchaguzi Mkuu wa 2015 na CCM wanapaswa kujipanga kuondoka madarakani.

Alitoa kali alimpotaja Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa kuwa Rais na Freeman Mbowe, Waziri Mkuu. Wengine aliowataja na kuwapa vyeo ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Waziri wa Fedha), Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Kilimo), Lema (Mambo ya Ndani), John Mnyika (Nishati) na Wenje (Mambo ya Nje).

LADY JAYDEE AWACHANA TENA CLOUDS.....ANADAI KWAMBA MUNGU SI "RUGE" WALA "KUSAGA"


Baada ya kipindi kirefu cha kuongea kwa mafumbo dhidi ya wamiliki wa Clouds FM kuwanyonya wanamuziki akianzia na wimbo wake wa Joto Hasira, mwanamuziki Judith Wambura ameendelea kuishambulia redio hiyo na leo Jumapili ameamua kufunguka kwa kuwachana  live  wamiliki wa redio hiyo.
Hii  ni  post  yake  aliyoipost   twitter:

Lady JayDee ‏@JideJaydee 1h
 
Naamini kabisa kuwa Mungu sio Ruge wala Kusaga. Atanisimamia kwenye hili #Confidence

ALICHOKISEMA ROMA MKATOLIKI KUHUSU NGOMA MPYA YA AFANDE SELE,

Rapper kutoka TANGA, Roma Mkatoliki ameisifia sana ngoma mpya ya msanii kutoka MOROGORO, Afande Sele ... Roma alifanya hivyo katika moja ya mtandao wa jamii anaotumia na kuandika ni ngoma ambayo ameisikilza mara 80 mpaka sasa na kuielewa sana ...
Ngoma hiyo mpya, ambayo AFANDE amemshirikisha BELLE 9 inajulikana kama DINI TUMELETEWA imeonekana kumgusa sana ROMA mpaka kuandika hivyo ...
Katika maneno yake, ROMA pia hakuacha kuongea na wasanii wenzie na fans kwa ujumla juu ya ngoma kama hizi kupewa kipaumbele ...
ROMA, "HII NGOMA MPYA YA AFANDE SELLE ft.BELLE 9 -Dini tumeletewa!!!
nimeisikiliza kama mara 80!! ina hisia sana na ni ngoma kali sana...!!!

HEY NIGGA IFIKIE KIPINDI NINYI MASHABIKI WETU NASISI WASANII TUFANYE HIZI NGOMA ZETU KALI NA ZENYE UJUMBE KAMA HIZI ZIHIT SANA HATA KAMA HAZITAPEWA NAFASI KATIKA RADIO STATIONS AU TV STATIONS!!!

Mwambieni afande ametisha sana humu ndani....oiii abelnego...big up 9/9/RIJEMBE!!!
"
BIG UP !! 

Tukio la kutekwa Ludovick ladaiwa kuwa ni 'feki' Polisi washikwa kigugumizi

*Tukio la kutekwa Ludovick ladaiwa kuwa ni 'feki'
*RB yake yazua utata, Polisi washikwa kigugumizi

JIMEIBUKA hofu ya kuwepo mpango mahususi unaoratibiwa na Serikali kufichua njama za kigaidi, ambazo zinadaiwa kutekelezwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaoheshimika katika jamii, MTANZANIA Jumapili limebaini.Taarifa za uhakika zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa, kukamatwa kwa mtuhumiwa namba mbili katika kesi ya ugaidi iliyofunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Ludovick Joseph, ni utekelezaji wa mpango huo.

Imedaiwa kuwa, kuna utata mkubwa wa usahihi wa taarifa za tukio la Ludovick kutekwa na watu ambao hawajafahamika hadi sasa na hata taarifa za kutekwa kwake alizodai kuzifikisha katika kituo kidogo cha polisi Kigogo, nazo zina utata.

Kwa mujibu wa wapasha habari wetu, taarifa za kutekwa kwa Ludovick na kunyang’anywa vitu vyake vyote alivyokuwa navyo, zikiwemo nguo alizokuwa amevaa na hata madai kuwa aliripoti tukio hilo katika kituo cha Polisi Kigogo siyo za kweli, bali zimetengenezwa ili kufanikisha mpango huo.

Ludovick alidai kutekwa usiku wa Jumanne ya Machi 5, mwaka huu, akiwa eneo la Sinza ambako alisema alitoa taarifa zake katika Kituo cha Polisi cha Kigogo na kufunguliwa RB yenye namba KIG/RB/318/2013.

Taarifa ya kutekwa kwake aliiandika mtandaoni na ilisomeka hivi; ‘Leo usiku, yapata saa tano na nusu, niliachana na Maggid Mjengwa maeneo ya Shekilango tukitokea Rose Garden. Yeye alielekea hotelini alikofikia sehemu fulani Kariakoo nami nikasubiri kigari kuelekea nyumbani kwangu.

Hapo Shekilango, magari yalichelewa kidogo, pembeni ilipaki bajaji ikiwa na watu wawili na dereva ndipo wakaniambia twende tuchangie mia tano tu kwenda Ubungo Mataa, nikakaa katikati ya hao jamaa.

Ghafla wakakata kona na kuanza kuelekea Mabibo huku wakiulizana kama wako kamili na mwingine kujibu yuko kamili. Nikajua tayari niko mikononi mwa majambazi na sikujua wako kamili namna gani, kwa hiyo nikaamua kuwa mtulivu.

Tulipofika relini karibu na Mabibo wakanipokonya begi lakini, hawakulifungua. Ndani yake kulikuwa na laptop, toshiba kubwa na chaji yake, kamera ndogo ya digital na USB yake, modem ya zantel na card reader. Tulipofika maeneo ya Loyola Sekondari, nikawasihi wanishushe ili nirudi mwenyewe, wakaniambia safari ile inaishia Jangwani.

Nikaingiwa na wasiwasi mkubwa na nia yao hasa, maana wameshanipokonya begi kwa nini wasiniachie? Lakini niliendelea kuwa mtulivu ili kutowaprovoke.

Tulipovuka Kigogo mwisho kwenye giza karibu na msikiti, wakasimama pembeni ya barabara na kuniamuru kushuka, nikashuka na kuanza kuwadai begi langu, ndipo mmoja akasema wamekuwa wastaarabu mimi naanza kuwadharau. Ghafla akanivuta kwa nguvu kunirudisha kwenye kibajaji akamwambia mwenzie wanisachi kama nina vitu vingine, wakanisachi na kuchukua pesa, nilikuwa na elfu 35 na simu mbili ndogo za nokia moja yenye line mbili.

Kisha mmoja akatoa ‘order’ nivuliwe nguo. Nikavuliwa viatu, T-shirt na suruali nikabaki na nguo za ndani pekee. Wakanishusha na kuniacha hapo.

Kurudi nyuma kama hatua kumi tu ndipo kituo kidogo cha polisi Kigogo nikaanza kutoa maelezo hapo kwa zaidi kama ya saa mbili nikiwa uchi na nguo za ndani tu. Nikiwa hapo nikasikia polisi wakiwasiliana juu ya tukio la kupigwa vibaya Absalom Kibanda, kwenye redio calls.

Ilikuwa yapata saa nane, baada ya kuchukuliwa maelezo polisi walinipatia gari nikaelekea hotelini kwa Maggid, ambaye saa kumi aliamshwa na kunichukulia chumba hapo nikapumzika. Ameniazima nguo zake ndizo nimevaa bado hadi sasa naelekea kituo cha Polisi Magomeni kwenda kupewa mpelelezi wa kesi yangu. Namba ya kesi yangu Kigogo ni KIG/RB/318/2013, wizi kutoka maungoni.’

Wakati Ludovick akiwa ametoa maelezo hayo kwa jamii kupitia mitandao ya kijamii, polisi wameshindwa kuthibitisha taarifa za kutekwa, kuporwa na kupokea taarifa yake aliyodai kuitoa kituo kidogo cha polisi Kigogo.

Polisi katika kituo kidogo cha Kigogo waliohojiwa na MTANZANIA Jumapili kuhusiana na taarifa za Ludovick, walionekana kurushiana mpira kuzizungumzia.

Askari aliyekutwa kituoni hapo alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema taarifa za matukio mbalimbali hufunguliwa hapo, lakini huhamishiwa Kituo cha Polisi cha Magomeni kutokana na udogo wa kituo hicho, hivyo kumtaka Mwandishi kufuatilia suala hilo katika Kituo cha Polisi Magomeni.

Gazeti hili lilipofika Kituo cha Polisi Magomeni, kwa Askari Mpelelezi liliyeelekezwa kuwa anahusika na kesi ya Ludovick aliyetajwa kwa jina moja la Chuki hakuwepo bali lilipewa namba ya simu yake ya kiganjani na alipotafutwa, naye alikana kuhusika na suala hilo na kuelekeza atafutwe askari polisi aliyetajwa kwa jina la Lukwamba Sanga.

Alipopigiwa Sanga na kuulizwa kuhusu sakata hilo, kwanza alikiri kuwa yeye ndiye mpelelezi wa kesi hiyo na kueleza kuwa ni kweli Ludovick alifungua RB katika kituo cha Polisi cha Kigogo lakini hakuwa tayari kutoa namba ya RB hiyo.

Alieleza kuwa mwenye mamlaka ya kutoa namba hiyo ni Mkuu wa Upelelezi wa Kituo ambaye hata hivyo hakupatikana, lakini ofisa mwingine kituoni hapo alieleza kuwa namba hiyo inaweza kutolewa kwa idhini ya Kamanda wa Mkoa wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela.

Kamanda Kenyela alipotafutwa, alisema anahitaji muda kuipata namba hiyo, kwa sababu ana majukumu mengi hivyo atafutwe baadaye. Lakini alipotafutwa tena simu yake ya kiganjani ilikuwa haipatikani.

Hata alipopigiwa simu tena jana iliita mfululizo pasipo majibu.

Wachambuzi wa masuala ya saikolojia wanadai dalili zinaonyesha kuwapo kwa uwezekano wa Ludovick kushiriki tukio la kutekwa na kupigwa kwa Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.

Wanasema ni kawaida kuwa watu wanaojihusha na matukio ya aina hii, baada ya kuyatekeleza huchanganyikiwa, hivyo hata kitendo cha Ludovick kukimbilia kuandika katika mtandao wa ‘facebook’ kuwa naye alitekwa kinaweza kuchukuliwa katika mtizamo huo.

Maswali ya kujiuliza
Ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja sasa baada ya kuvamiwa na kuteswa kwa Kibanda na siku chache baadaye kukamatwa kwa Ludovick akihusishwa na tuhuma za kupanga ugaidi, yapo maswali mengi miongoni mwa jamii ambayo hayajapata majibu kuhusu matukio hayo.

Swali kubwa linaloumiza vichwa vya wengi hivi sasa ni namna ambavyo Ludovick alifanikiwa kujipenyeza na kufanikiwa kujenga mtandao wa masiliano ya simu za mkononi na katika mitandao ya kijamii na Wahariri mbalimbali wa Vyombo vya Habari.

Tayari Wahariri wawili, Deodatus Balile na Ansbert Ngurumo, wamekwishatajwa kuwa na mawasiliano ya muda mrefu na Ludovick na kwamba kuna baadhi ya taarifa muhimu za waandishi na wahariri ambazo Ludovick alikuwa akizipata kupitia mawasilino yake hayo.

Kutajwa kwa wahariri hao kuwa washirika wa karibu kimawasiliano na Ludovick, kuliibua hisia kuwa Wahariri hao, waliingizwa katika mtandao wa Ludovick na kuanza kufanya kazi zake pasipo wao wenyewe kujua au wakiwa na ufahamu huo.

Lakini pia wadadisi wa mambo wamekuwa wakihoji nguo za Ludovick zilipo baada ya kile kinachodaiwa kuwa tukio hilo la kudai kutekwa ni feki.

Hali kadhalika hatua ya Ludovick baada ya kuachana na Mjegwa na kupanda bajaji iliyokuwa na watu wawili kisha akakaa katikati kwa nauli ya shilingi mia tano huku akiwa na pesa taslimu shilingi 35,000, begi lenye laptop toshiba kubwa, chaja yake, kamera ndogo ya digital na USB yake, modem ya zantel na card reader, jambo linaloonyesha kuwa alikuwa na uwezo wa kuchukua usafiri salama zaidi.

Aidha, mkanganyiko wa maelezo ya Ludovick na yale yaliyotolewa na Mjengwa ambako yeye (Ludovick) alidai kupewa gari na polisi kumpeleka hotelini kwa Maggid, huku Maggid akidai alifika hapo kwa usafiri wa teksi, nayo yanazidi kuacha swali gumu la kupata ukweli wa sakata hili zima.

Kuhusishwa kwake na tukio la Kibanda Siku na wakati ambao Kibanda alitekwa na kuteswa, Ludovick naye alidai kutekwa na majambazi akiwa eneo la Sinza, jirani na mahali ilipo ofisi ya Kibanda. Ludovick alidai kutekwa na watu wasiojulikana majira ya saa tano usiku siku ya Jumanne ya Machi 5, mwaka huu, ambapo watekaji wake walimnyang’anya vitu vyake mbalimbali na kumvua nguo zote pamoja na kuchukua simu zake mbili.

Ingawa katika uchunguzi wake gazeti hili liliambiwa kuwa simu yake iliendelea kutumika katika maeneo ya mnara wa Sinza karibu na ofisi anakofanyia kazi Kibanda siku mbili mara baada tukio la kuteswa kwa Mhariri huyo. Pamoja na hilo, siku mbili kabla Kibanda hajatekwa, anadaiwa kufanya mawasiliano na kiongozi mmoja mkubwa wa chama cha siasa.

Ahusishwa na video ya Lwakatare
Yuko mikononi mwa sheria na alishafikishwa Mahakamani pamoja na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare, kutokana na mipango ya kudhuru watu, wakiwemo waandishi wa habari pamoja na suala la ugaidi.

Inaelezwa kuwa watu hao wamekuwa karibu kwa muda mrefu ambapo wote ni wenyeji wa Mkoa wa Kagera, na kwa mujibu wa watu wa karibu na mahusiano yao, walisema kuwa Ludovick amepata kumsaidia kufanya kampeni za kuwania ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini mwaka 2000.

Ludovick ni nani?
Ludovick, mbali na kuwa na ukaribu na Lwakatare, pia alikuwa mtu wa karibu na Mjengwa, akimsaidia katika shughuli za blog yake, pamoja na wahariri mbalimbali wa habari.

Ludovick pia wapo wanaomtambua kama mtu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Mjengwa pia aliwahi kukiri kutofahamu kazi halisi aliyokuwa akiifanya Ludovick mtaani, lakini katika maelezo yake aliyoandika kupitia kwenye mtandao wa Jamii Forum, Mjengwa alisema anamfahamu Ludovick tangu akiwa Chuo Kikuu (DUCE) na kwamba ni mmoja wa Watanzania wengi waliomfahamu kupitia kazi zake magazetini.

WABUNGE WACHACHAMAA JUMBA LA MCHUNGAJI LWAKATARE LIVUNJWE


'Hekalu' linalomilikiwa na Mchungaji Getrude Lwakatare.

Wabunge wamemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Terezya Huvisa kuzivunja nyumba mbili zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam zilizojengwa katika fukwe ya bahari ya Hindi ikiwemo ya mbunge licha ya kwamba kuna zuio la mahakama.

Bila kutaja majina ya wamiliki hao, wabunge hao walitaka hatua hizo zichukuliwe kwa haraka kwa nyumba hizo zilizojengwa kwenye fukwe kinyume cha sheria zivunjwe kwa maelezo kuwa hazina ofa wala hati.
 
Sambamba na hilo wametaka watendaji wa serikali waliohusika kutoa vibali kuruhusu ujenzi huo kwa maelezo kuwa walichukua rushwa wachukuliwe hatua.
 
 Mbunge wa kwanza kuanza kuzungumzia hilo ni wa viti maalum, Esther Bulaya (CCM) aliyetaja viwanja viwili vyenye namba 2019 na 2020 kikiwemo cha mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani waliojenga  nyumba zivunjwe licha ya kuwepo zuio la mahakama.
 
 “Mwaka jana waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka alivunja nyumba za kawaida licha ya zuio la mahakama, lakini nyumba zilizo kwenye viwanja namba 2019 na 2020 hazikuvunjwa kwa sababu ya zuio la mahakama hii ni double standard hatuwezi kuvumilia. 
“Wengine wenye nyumba ni viongozi tupo nao humu tena wa kiimani, lakini kwa nini viongozi tunafaya hivi wakati tunatakiwa tuwe wa mfano na tunawafanya viongozi wenzetu washindwe kufanya kazi zao?…hakuna haja ya kuogopa waziri Huvisa (Mazingira) vunja nyumba, haiwezekani kuwa na nguvu ya fedha.
 
 “Wabunge wenzangu tuazimie Manispaa ya Kinondoni na NEMC (Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira), wakavunje nyumba hizo ndani ya wiki moja , naomba kutoa hoja,” alisema.
 
 Hata hivyo, Spika Anne Makinda alimweleza; “Haiwezekani kutoa hoja kwa kuingilia vyombo vingine”.
 
 Mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani mwenye nyumba katika  eneo hilo la Mbezi Beach aliyejenga katika fukwe ya bahari kwa kuondoa mikoko na kuweka kifusi na kujenga nyumba ni Mbunge wa Viti Maalumu, Mchungaji Dk. Getrude Lwakatare (CCM).
Naye Mbunge wa viti maalumu, Grace Kiwelu (Chadema) akichangia bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, alisema kamati yake ya Ardhi na Mazingira ilitembelea eneo hilo la Mbezi Beach na kukuta aliyejenga katika kiwanja 2019 hakuwa na ofa wala hati.
 
 “Ametumia pesa kuwarubuni watendaji akaondoa mikoko, akaweka kifusi na akajenga nyumba naomba wizara ya Ardhi na ya mazingira wawachukulie hatua watendaiji hao,” alisema. 

Akijibu hoja ya Bulaya, kuwa kwanini nyumba ya Mchungaji Lwakatare haikuvunjwa wakati nyingine zilivunjwa, mwanasheria mkuu wa Serikali, Frederick Werema alisema: 
 
“Sisi ni wajibu wetu twende mahakamani kusema watu hao wamevunja sheria kujenga hapo. Wao wanaruhusiwa na Katiba na mahakama itafuata sheria.

“Nashauri Bulaya usitoe shilingi kuzuia Bajeti ya Waziri, uje tuone huyo kigogo itakuwaje.” 
Hata hivyo, Huvisa alisema: “Nyumba tulizovunja hazikuwa na kesi na hii tuliyoiacha ilikuwa na kesi.”
Jumba la kifahari linalodaiwa kuwa la Mchungaji Lwakatare ambalo lilizinduliwa mwaka jana, limekuwa klikitajwa kuwa lina thamani ya takribani sh bilioni 1.5.
zero99

Saturday, April 20, 2013

Kwanini Serukamba Hakutolewa Bungeni?

Nyerere: "waswahili wana mambo ya ajabu. mambo ya kijinga jinga yakisemwa kwa kiingereza, wanashangilia kana kwamba ni mambo mema"

Hayo ni baadhi ya maneno aliyoyasema baba wa taifa Mwl Julius K. Nyerere katika moja ya hotuba zake.
Tusi alilolitoa Serukamba ndio tusi kubwa kuliko yote yaliyowahi kutolewa bungeni mpaka sasa. Tofauti na mengine yeye lake amelitoa kwa kiingereza kiasi kwamba naibu spika ameliona ni jema hivyo kutomchukulia hatua yoyote.

Hata majadiliano yanayoendelea sasa miongoni mwa wananchi na viongozi ni kuhusu "utovu wa nidhamu" wa Tundu Lissu wa kuomba miongozo na taarifa kila mara hivyo kutimuliwa bungeni na wenzake waliokuwa wakipinga kitendo cha naibu spika kumtoa nje. Hili la Serukamba halizungumzwi kama ni tusi kuu bungeni.

Tatizo ni kama alivyosema Nyerere, katukana kwa kiingereza hivyo spika na naibu wake hawaoni kuwa ni tusi. Waziri mkuu haoni kuwa ni tusi. Aibu!

KAULI YA JUMA NATURE BAADA YA KUTIMULIWA EATV BAADA YA KUINGIA AKIWA AMEVAA KANDAMBILI


.
.
.
.

"SPIKA WA BUNGE ANALIONGOZA BUNGE KWA " REMOTE CONTROL" TOKA NJE.....HII NI KAULI YA DR. SLAA


Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa amesema Spika wa Bunge Anne Makinda amekinajisi kiti cha spika.

Dr Slaa ambaye ni gwiji wa siasa za Tanzania amemshutumu vikali Spika na Naibu wake kwa kuharibu kabisa bunge la Tanzania na kupoteza kabisa heshima yake ndani na nje ya nchi.


Dr Slaa amefichua kwamba maamuzi yote yanayofanywa na Anne Makinda si kwa utashi wake bali ni kutokana na maelekezo maalum anayoelekezwa kutoka nje ya bunge.


Kutokana na vitendo vinavyofanywa na kiti cha Spika imefika mahali Spika na Naibu wake wanadharauliwa hata na watoto wadogo.


Spika Anne Makinda kwa sasa ni mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri kuu ya CCM.


Source:ITV Habari.

‘Viroba’ tishio jipya saratani ya koo kwa wanaume

 

Daktari bingwa wa uchunguzi wa magonjwa ya saratani katika Kitengo cha Patholojia, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk Henry Mwakyoma na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk Crispin Kahesa wameeleza hayo jijini Dar es Salaam.
Walisema kuwa ingawa bado hakuna visababishi kamili vya saratani hiyo, asilimia 90 ya wagonjwa wa saratani ya koo wamekuwa na historia ya uvutaji sigara, unywaji pombe kali kama viroba na kula aina za vyakula vilivyochomwa ikiwamo nyama na samaki, ulaji pilipili, ndimu, ‘chilisosi’ na unywaji wa vitu vya moto kupita kiasi.
“Ongezeko ni kubwa, asilimia 90 ya wagonjwa tuliowapokea hapa wana historia ya kutumia vilevi vikali, sigara, pilipili kwa wingi na aina nyingine na vitu vinavyosababisha saratani hii,” anasema Dk Kahesa.
Anasema kuwa Saratani ya Koo ni mbaya zaidi ukilinganisha na saratani za aina nyingine.
Anaeleza: “Saratani ya Koo ni mbaya ukimwona mgonjwa unaweza kulia, hawezi tena kula na ikibidi huingiziwa mipira maalumu ili kupitisha chakula, lakini kuna wakati hata mipira huziba, hivyo huishi kwa dripu ya chakula pekee.”
Naye Dk Mwakyoma anaeleza kuwa Saratani ya Koo hushambulia seli zinazotanda koo na kutengeneza uvimbe katikati ya koo ambao huanza kuleta madhara taratibu.
“Ukiwa na Saratani ya Koo, itakuchukua muda mrefu sana mpaka kuanza kuona viashiria mbalimbali, awali mgonjwa huanza kupata shida kumeza chakula. Wengi hufika hapa wakiwa wamechelewa na tunavyofanya vipimo huwa katika hatua mbaya sana,” anasema Mwakyoma.
Anazitaja aina kuu mbili za Saratani ya Koo kuwa ni: “Oesophagus Carcinoma na Squamous cell carcinoma, ambazo hutofautiana kulingana na jinsi seli zake zinavyoonekana kwenye darubini.
Hata hivyo, pamoja na tofauti hizo za mwonekano, utambuzi na matibabu ya aina hizi za Saratani ya Koo hufanana.”
Anabainisha kuwa aina zote mbili huanza kwa kuathiri seli zilizo katika utando wa ndani wa ukuta wa koo, uitwao ‘mucosa’ kabla ya kusambaa maeneo mengine.
Kwa upande wake Dk Kahesa anasema kuwa katika hatua za awali, mgonjwa mwenye Saratani ya Koo anaweza asionyeshe dalili zozote. Hata hivyo, kadiri saratani inavyozidi kukua na kuenea, mgonjwa anaweza kuanza kuona dalili.
“Dalili ya kwanza ya mgonjwa wa saratani ni chakula kukwama kwenye koo, siku za mwanzo mgonjwa anaweza kushindwa kumeza chakula kigumu kisha cha majimaji na baadaye akashindwa kumeza hata mate.