Monday, April 22, 2013

BABY MADAHA: NTAWACHANGANYA WANAUME KAMA DIAMOND


STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ amesema mwaka huu atawachanganya wanaume kama afanyavyo Nasibu Abdul ‘Diamond’ ili kwenda sawa.
Akifafanua kauli yake kwa paparazi wa Stori 3, Baby Madaha aliweka bayana kuwa haoni tatizo kunaswa na Mwisho Mwampamba kama ilivyoripotiwa hivi karibuni wakati huohuo anatoka kisela na mkali wa Bongo Fleva, Juma Kassim ‘Nature’.
“Watakoma mwaka huu, lazima niwachanganye sana, mbona wao wanatuchanganya sana kama Diamond vile anavyofanya!” alisema Baby.




Love to hear what you think!