UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na
tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya
mapenzi kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi
Imefahamika kwamba
vijana hao, kaka na dada wamenaswa ‘wakingonoka katika mapango
yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Tukio
zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara
kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska
usiku na mchana.
Risasi lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.
Haikufahamika
mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu
katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu
alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.
Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata
hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa
akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera
zetu.
Ni kama vile hawakuwa na makubaliano na kile walichokuwa wakienda kukifanya.
Mara
kadhaa dada huyo alionekana kumkwepa kaka yake na alikuwa akijiondoa
karibu yake pale alipomlazimisha kutaka kumfanyia kitu kisichokuwa cha
kawaida.
Kamera za Risasi ziliwafuatilia wawili hao kwa kuwa walionekana kuwa na kitu ‘spesho’.
Mpaka
wanazama katika mapango yaliyopo kando ya ufukwe huo wa Coco, kamera
zilikuwa zikiendelea kuwachukua hadi walipozama ndani kabisa ya mapango
hayo.
Walipozama ndani ya mapango hayo, ghafla walitokea askari ambao nao walikuwa wakifuatilia nyendo za wawili hao.
Askari
hao wa Kituo cha Oysterbay, wakiongozwa na kamanda wa oparesheni
maalumu katika Wilaya ya Kinondoni, Kamanda Swai walifuatilia kwa
umakini tukio hilo.
Wakiwa chini ya mapango, kaka na dada
waliondoa vinguo vilivyokuwa maungoni mwao na kuanza kuduu kama vile
walikuwa katika ufukwe unaoruhusiwa kufanya vitendo hivyo.
Kabla
askari hawajawavamia, waliwashuhudia wawili hao wakiwa katika kilele cha
sterehe yao huku dada mtu akionesha kutoa ushirikiano kwa shingo
upande.
Ghafla, askari waliwavamia na kuwatibulia starehe yao kisha kuwatia mbaroni.
Baada
ya kuona kuwa wamevamiwa na askari, kaka mtu alichomoka na kutafuta
silaha ili kuweza kujihami na wavamizi wake bila ya kujua kama ni
askari.
Katika hilo nusura zipigwe kati ya askari na kaka huyo
ambaye alikuwa akitaka kupigana na watu asiowajua kwa kuwa walikuwa
wametinga mavazi ya kiraia.
Hata hivyo, alitulizwa na kutakiwa kuvaa pensi yake ili aweze kutoa maelezo kwa kina.
Wakati
yote yakiendelea, dada mtu alikuwa amepigwa na butwaa na kutojua cha
kufanya hadi aliporushiwa kitenge chake kilichokuwa pembeni ili
ajisitiri mwili wake.
Katika mahojiano ya awali yaliyoongozwa na Kamanda Swai, ilibainika kwamba wawili hao ni ndugu wa damu yaani kaka na dada.
Maelezo
hayo yanasema kuwa dada mtu alitoka mkoani na alikuja kutembea jijini
Dar es Salaam, ndipo kaka yake alipomtaka watoke kwenda kumuonesha
vivutio vya jiji hilo.
“Nina miaka 19, nimetokea Iringa kuja Dar
kutembelea familia lakini kaka akanileta huku na kunifanyia vile, siyo
kama tulikuwa tumekubaliana,” alisema dada huyo kwa aibu.
Kaka mtu alikiri kile kilichosemwa na dada yake na kushindwa kujitetea kwa kuwa kila kitu kilikuwa hadharani.
Wawili
hao walichukuliwa na kupelekwa katika Kituo cha Oysterbay kwa ajili ya
kufunguliwa kesi ya uzembe na uzururaji na kusekwa rumande kabla ya
kufikishwa mahakamani.
GPL