Sunday, April 21, 2013

ALICHOKISEMA ROMA MKATOLIKI KUHUSU NGOMA MPYA YA AFANDE SELE,

Rapper kutoka TANGA, Roma Mkatoliki ameisifia sana ngoma mpya ya msanii kutoka MOROGORO, Afande Sele ... Roma alifanya hivyo katika moja ya mtandao wa jamii anaotumia na kuandika ni ngoma ambayo ameisikilza mara 80 mpaka sasa na kuielewa sana ...
Ngoma hiyo mpya, ambayo AFANDE amemshirikisha BELLE 9 inajulikana kama DINI TUMELETEWA imeonekana kumgusa sana ROMA mpaka kuandika hivyo ...
Katika maneno yake, ROMA pia hakuacha kuongea na wasanii wenzie na fans kwa ujumla juu ya ngoma kama hizi kupewa kipaumbele ...
ROMA, "HII NGOMA MPYA YA AFANDE SELLE ft.BELLE 9 -Dini tumeletewa!!!
nimeisikiliza kama mara 80!! ina hisia sana na ni ngoma kali sana...!!!

HEY NIGGA IFIKIE KIPINDI NINYI MASHABIKI WETU NASISI WASANII TUFANYE HIZI NGOMA ZETU KALI NA ZENYE UJUMBE KAMA HIZI ZIHIT SANA HATA KAMA HAZITAPEWA NAFASI KATIKA RADIO STATIONS AU TV STATIONS!!!

Mwambieni afande ametisha sana humu ndani....oiii abelnego...big up 9/9/RIJEMBE!!!
"
BIG UP !! 



Love to hear what you think!