UJERUMANI imetoa kipigo cha bao 4-0 kwa Ureno katika mechi ya kundi G
ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Mabao ya Ujerumani yamewekwa
kimiani na Thomas Muller aliyefunga hat-trick na la nne likifungwa na
Mats Hummels. Katika mechi hiyo, Pepe wa Ureno alizawadiwa kadi nyekundu
baada ya kumpiga kichwa Muller.