HAIWEZI kuwa aibu mpaka siri ifichuke, kwa wake za watu 13 walionaswa
wakijiuiza, kwao imekuwa zaidi ya kuumbuka, wametia fedheha ndani ya
familia zao.
Wake hao za watu, walinaswa usiku wa Jumanne iliyopita,
Barabara ya Shekilango, kuanzia Afrika Sana mpaka Mori, Sinza, Dar es
Salaam, wakati jeshi la polisi lilipofanya msako maalum wa kushtukiza.

Pamoja
na wake hao za watu, vilevile wanafunzi 18 wa vyuo mbalimbali nchini,
mahausigeli saba na mabaamedi watano, arobaini yao ilifika siku hiyo,
walipokamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Kijitonyama, Mabatini kabla
ya kupandishwa kizimbani, Mahakama ya Jiji siku iliyofuata.
Katika
msako huo, zaidi ya makahaba 60 walikamatwa na katika mahojiano na
polisi, ikabainika kuwapo kwa wake hao za watu, wanafunzi, wahudumu wa
baa na wafanyakazi wa ndani.
WAKE ZA WATU.......
Jeshi
la polisi likichukua maelezo ya mmoja baada ya mwingine, askari mmoja
alimfikia mwanamke aliyefahamika kwa jina la Suzan Moses ambaye katikati
ya mahojiano, alijieleza kwamba ni mke wa mtu.

Suzan ambaye baadaye
ilibainika kwamba hujulikana pia kwa jina la Mamaa Suzy, alijieleza kuwa
anaishi na mume wake Tandale, Dar es Salaam na wana
watoto wawili.
Askari aliyekuwa anamhoji Suzan, aliuliza: “Mke wa mtu kweli na watoto wawili unajiuza, huoni kama ni hatari?”
Suzan: “Hatari naijua ndiyo maana simruhusu mwanaume yeyote aniingilie bila kondomu, nipo makini juu ya hilo.”
Askari: “Mumeo anajua kama unajiuza?”
Suzan:
“Hajui, japokuwa hata yeye tulikutana viwanja.
Nilimdanganya mimi ni
mhudumu wa Corner Bar, akaniachisha kazi lakini baada ya kuona
hanitimizii mahitaji muhimu, nikamwambia narudi kazini, kwa hiyo mpaka
leo anajua nahudumia baa.”
Baada ya wote kuhojiwa, ikabainika kuwa
katika wanawake hao 60 waliokamatwa, mbali na Suzy, walikuwepo wengine
12 ambao ni wake za watu.
Mwanamke
mwingine, Jessica Mashaka alidai kuwa aliamua kujiuza baada ya kubaini
kwamba mume wake analelewa na mwanamke mmoja tajiri jijini Dar es
Salaam.
“Anachokifanya mume wangu ni sawa na mtu anayejiuza. Akipewa
fedha na mwanamke wake ananinyanyasa ndani ya nyumba, nikaona na mimi
nijiuze nipate fedha zangu mwenyewe ili aache kuninyanyasa.”

Hata
hivyo, Leila Madaha alidai yeye na mume wake walikubaliana ajiuze ili
wawe wanapata fedha za kujikimu.
Alisema: “Mume wangu huwa ananisisitiza
kutumia kondomu kwa kila mteja, yeye hana kazi tangu alipofukuzwa
bandarini miaka minne iliyopita.”
WANAFUNZI......
Wanafunzi 18 kutoka vyuo vya Dar es Salaam, Dodoma na Iringa, walijitambulisha katika mahojiano na hayo na polisi.
Wanafunzi wa
mikoani walisema kuwa hali ni mbaya kibiashara huko tangu iingie
Januari ndiyo maana wamekuja Dar kujaribu kutafuta kipato.
MABAAMEDI NA MAHAUSIGELI.......
Katika
wanawake hao, ilibainika wapo mabaamedi watano ambao walidai kuwa
vipato vyao ni vidogo ndiyo maana kila baa wanazofanyia kazi
zinapofungwa saa 5:00 usiku, hulazimika kuingia mitaani kuuza miili
waweze kupata fedha zaidi za kuwawezesha kuishi.
Vilevile, wapo
mahausigeli saba ambao maelezo yao yalikuwa sawa na yale ya mabaamedi
kwamba hulipwa ujira mdogo na mabosi wao ndiyo maana hulazimika kujiuza
ili kuongeza vipato.