Thursday, January 17, 2013

"RAY HAIJUI HATA NGUO YANGU YA NDANI....NAOMBA NIWEKE WAZI KUWA SI MPENZI WANGU"...SAJENT


BAADA ya ishu kuvuja kuwa msanii wa filamu Husna Idd ‘Sajenti’, ana mahusiano ya kimapenzi na ’Ray’, amezikana habari hizo huku akisisitiza kuwa msanii huyo anamchukulia kama kaka yake na suala la kutoka naye kimapenzi halina ukweli wowote.

Tukio la Sajenti kutoka na Ray lilianza kuskika pindi kundi la bongo movie lilipoenda mkoani Mwanza kucheza mchezo wa kirafiki na wasanii wa mkoani humo.


Mtandao huo ulitaka kujua Sajenti anazungumziaje habari hizo, ambapo alidai kuwa hajawahi kutoka na  ’Ray’  kimapenzi na anayesambaza ishu hizo ana nia ya kumchafua ingawa alishindwa kueleza anachafuliwa kwa namna gani.


Alisema kuwa kama zingekuwa na ukweli taarifa hizo angeweka wazi lakini haoni sababu ya kukubali wakati kitu hajawahi kukifanya na wala hana wazo wa kutoka na msanii huyo kwani mpenzi wake anamtosha.


“Sijawahi kutoka kimapenzi na  Ray na  hajui  hata  nguo yangu ya  ndani na kama una ukweli kama unajua natoka naye kwanini umepiga simu na kuniuliza,??.. nasema sijawahi kutoka naye,” alidai.

Hata hivyo msanii huyo aliongeza kuwa kama mwanaume aliwahi kutoka naye hawezi kuficha lakini juu ya Ray atakanusha siku zote.



Love to hear what you think!