Monday, September 16, 2013

PICHA za mwigizaji Flora Mvungi (Hadija) ambaye ni mke wa msanii Hamis Baba ‘H. Baba’ akijifungua mtoto wa kike baada ya kusota kwa muda mrefu ZIMEVUJA

 
 Flora Mvungi (Hadija) akijifungua.
Kutoka kwa vyanzo vyake, mbali na picha za mtoto, Mwandishi wetu alilibamba tukio la Flora akijifungua Jumatano iliyopita katika Hospitali ya Marie Stopes iliyopo Sinza, Dar.


Flora akiwa hospitali na mumewe H. Baba.
Kwa mujibu wa H. Baba, alifurahishwa kuitwa baba kwani ni kitu ambacho alikuwa anatamani kwa muda mrefu na Mungu amemtimizia hivyo anamshukuru kwani ni zawadi kubwa katika maisha yake.


Mtoto wa Flora Mvungi.
Kwa upande wa Flora alikuwa na haya ya kusema: “Namshukuru sana Mungu kwa sababu niko salama na mwanangu, ukweli mwacheni mama aitwe mama kwani kuzaa siyo kazi rahisi”.
 

H. Baba alimalizia kwa kusema kuwa kama walivyosema awali kabla mtoto huyo hajazaliwa kuwa jina lake ataitwa Tanzanite, ndiyo hivyo itakavyokuwa jina hilo ndilo litakalotumika.



Love to hear what you think!