Wednesday, February 13, 2013

PICHA YA WEMA SEPETU "AKIPIGWA MATE" NA NJEMBA NYINGINE TENA


STAA wa filamu mwenye jina kubwa Bongo, Wema Abraham Sepetu, juzikati alitupia picha yake akiwa kimahaba zaidi na mwanaume aliyedai kuwa ni ‘mume’ wake.

Picha hiyo ambayo aliiweka kwenye mtandao wa BBM inamuonesha msanii huyo akibusiana na mwanaume huyo lakini wakionekana kuanzia kwenye kidevu hadi kwenye kiuno.

Baada ya kuitupia picha hiyo, Wema aliandika: ‘Miss you mume wangu, wewe ndio kila kitu katika maisha yangu, watasema sana lakini mambo yetu yanatuendea vizuri.” 


Maneno hayo yanaashiria kuwa Wema anampenda sana mwanaume huyo ambaye siyo Diamond.


Love to hear what you think!