Thursday, July 19, 2012

MECKY MEXIME KOCHA MKUU MPYA WA MTIBWA SUGAR


Baada ya kuiwezesha timu ya mkoa wa Mororgoro kubeba taji lake la kwanza la mashindano ya Copa Coca Cola, leo hii mchezaji wa zamani Mtibwa Sugar na nahodha wa Taifa Stars aliyepita kabla ya Nsajigwa - Mecky Mexime ameteuliwa rasmi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Manungu Turiani - Mtibwa Sugar.


Mecky Mexime ambaye mara baada ya kustaafu soka miaka kadhaa iliyopita alipata kibarua kwenye benchi la ufundi la Mtibwa kama kocha msaidizi - mapema mwezi huu aliiongoza timu ya mkaoa wa Moro kuwa mbabe wa mikoa yote ya Tanzania kwa kuchukua ubingwa Copa Coca Cola na matokeo yake uongozi wa mabingwa wa zamani wa Tanzania bara umeamua kumpa ajir kamili ya ukocha mkuu wa timu yao ambayo kwa misimu ya hivi karibuni imeonekana kutofanya vizuri kwenye michuano mbalimbali inayoshiriki.


Love to hear what you think!