Sunday, September 29, 2013

KIJANA APIGWA, ATELEKEZWA

Damian akiwa hajitambui baada ya kukutwa eneo la Ukonga Mazizini jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Wananchi waliofika kumshuhudia kijana Damian.
Askari Kanzu aliyejulikana kwa jina la Inspekta Leonard Luhende (mwenye simu) akifanya mawasiliano na polisi kwa lengo la kumpatia kijana msaada.
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Damian, mkazi wa Ukonga Mazizini jijini Dar es Salaam, amekutwa hajitambui kutokana na hali iliyonekana ni ya kupigwa. Kwa mujibu wa wananchi wa eneo hilo, kijana huyo anayedaiwa kupigwa na watu wasiojulikana, ametambuliwa kuwa ni mkazi wa hapo na pia anajishughulisha na biashara ndondogo katika soko la Karume, wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.



Love to hear what you think!