Monday, December 8, 2014

MAN UTD YATINGA TATU BORA LIGI KUU ENGLAND

Van Persie akiongea na mashabiki baada ya kufunga bao.
Mshambuliaji wa timu ya Southampton, Graziano Pelle akishangilia baada ya kufunga bao la kusawazisha kwa timu yake dhidi ya Man United dakika ya 31 kipindi cha kwanza.
Wachezaji wa Southampton wakishangilia kwa pamoja.
Beki wa Southampton Ryan Bertrand (kushoto) akipambana na Juan Mata (kulia).
Van Persie akishangilia baada ya kufunga bao la pili dakika ya 71 kipindi cha pili.
Kocha wa Man United, Louis van Gaal (kushoto) akisalimiana na Ronald Koeman (kulia).
Msimamo wa ligi hiyo kwa sasa.
MANCHESTER UNITED  usiku wa kuamkia leo imepanda hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kuwafunga  wapinzani wao Southampton kwa jumla ya magoli 2 - 1 katika mechi iliyopigwa kwenye uwanja wa St. Marys
Mshambuliaji wa Manchester United, Robin Van Persie ndiye aliyefunga magoli yote mawili kwa upande manchester United.
Kwa matokeo hayo Manchester inapanda hadi nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi hiyo na kuwashusha Southampton hadi nafasi ya tano.
Msimamo kwa sasa Chelsea wapo nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi hiyo, Manchester City ya Pili na Manchester United wapo nafasi ya tatu.
Southampton (4-2-3-1): Forster 5.5; Clyne 6, Fonte 5, Yoshida 6, Bertrand 6; Steven Davis 7, Wanyama 6.5; Long 6.5 (Mayuka 79, N/A), Tadic 6.5 (Hesketh 70, 6), Mane 6, Pelle 7.
Subs not used: Kelvin Davis, Gardos, , Isgrove, Reed, Targett.
Man Utd (3-5-2): De Gea 6.5; McNair 5 (Herrera 38, 6), Smalling 5.5 (Evans 16, 6), Rojo 6; Valencia 5.5, Carrick 6.5, Fellaini 5, Mata 4.5 (Fletcher 89, N/A), Young 5.5; Van Persie 8, Rooney 6.5.
Subs not used: Lindegaard, Falcao, Januzaj, Wilson.
Attendance: 31,420



Love to hear what you think!