Stori: Musa Mateja
NYOTA wa
Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye hivi karibuni aliripotiwa
kupokea kipigo cha maana kutoka kwa msanii mwenzake, Rashid Makwilo
almaarufu Chid Benz, ameibuka na kudai kuwa atahakikisha rapa huyo
anaozea jela kwa kitendo hicho alichomfanyia.
Akizungumza na gazeti hili, Ray C alisema amejikuta akipatwa na dhamira
hiyo kutokana na msanii huyo, licha ya yeye mwenyewe na mama yake
kumpigia simu za kutaka amsamehe, lakini anakana mbele za watu
anapoulizwa, tena hadi redioni.
“Chid na mama yake wamenipigia simu kutaka nimsamehe lakini ninashindwa
kwa sababu akiulizwa na watu anakataa hajanipiga, sasa kama hajanipiga
anaomba msamaha wa nini, nimekwenda kwao na polisi kama mara tano lakini
haonekani, inaonekana amejificha sehemu, mimi nasema awaonee haohao
wasiojua sheria,” alisema msanii huyo ambaye hivi sasa anaendesha vita
dhidi ya matumizi ya madawa ya kulevya.
Alipoulizwa kuhusu kauli hiyo, Chid Benz mwenye tuzo tano za Kili, licha
ya kukiri kumpigia Ray C simu pamoja na mama yake, alikataa kupiga kwa
ajili ya kuomba msamaha kwa sababu hakumpiga msichana huyo mkongwe
katika Bongo Fleva.
“Mimi nimpige Ray C? Halafu achubuke mguuni? Chid Benz angempiga
angepasuka sura na angevimba kila sehemu. Yeye anajua nini kilitokea
lakini anasema maneno yasiyokuwepo ilimradi apate huruma ya watu.
Nilishamkataza kuwa karibu na mzazi mwenzangu kwa kuwa najua kampuni
yake haina future.
“Mbona hasemi kama nilishawahi kwenda pale na kumweleza sitaki na akaniomba msamaha?
“Mimi sikumpiga, mchubuko alioupata ni mchecheto wake tu baada ya kujikwaa na kuanguka wakati akinikimbia, mimi nichukue cheni? Hayo ni mambo ya kizamani kwamba mtu ukimpatia sababu unasema amechukua pesa sijui na nini, siwezi kuchukua cheni ya Ray C, kwa maisha gani aliyonayo?
“Mimi sikumpiga, mchubuko alioupata ni mchecheto wake tu baada ya kujikwaa na kuanguka wakati akinikimbia, mimi nichukue cheni? Hayo ni mambo ya kizamani kwamba mtu ukimpatia sababu unasema amechukua pesa sijui na nini, siwezi kuchukua cheni ya Ray C, kwa maisha gani aliyonayo?
“Anasema nilimpigia simu kumuomba radhi, ni kweli lakini siyo kumwomba
radhi, nilimpigia na kumwambia tuachane na haya mambo, sisi wote
tunaonekana mateja tu mbele za watu ambao tumeshindwana huko sasa
tunataka publicity.
“Wanaosema mimi ni mkorofi hawanijui, kama ni hivyo mbona ile kesi ya
kumpiga msichana kule Ilala nimeshinda?” alihoji Chid Benz.