Thursday, February 13, 2014

BAADA YA KANISA LA WALA NYASI,KANISA JINGINE LA AJABU LAIBUKA,WAUMINI WANASALI WAKIWA UCHI WA MNYAMA

article-0-1B61B1AD00000578-28_634x358Kanisa lenye taratibu za ajabu za kuabudu limeibuka huko Virginia Marekani, ambapo waamini wake wameruhusiwa kuhudhuria ibada wakiwa uchikutokana na madai kuwa Waamini wa makanisa mengi sikuhizi wamekuwa wakishindana na kupeana hadhi kulingana na aina ya mavazi wanayoingia nayo katika ibada.

article-0-1B61B0F700000578-550_634x352  
Kiongozi wa kanisa hili (White Tail Chapel), Pastor Allen Parker amesema kuwa ameamua kuwaruhusu waumini wa kanisa lake kuingia kanisani bila nguo ili kuweka usawa kati yao mbali na mavazi na vitu vya kidunia.
Pastor Allen pia amekuwa akisimamia mafundisho yake haya kwa kuzingatia hadithi za Maandiko Zikiwepo za Adam na Hawa kukaa uchi katika bustani ya Eden bila aibu, Kuzaliwa bila kuwa na nguo pamoja na mambo mengine yanayofanana na hayo.article-0-1B61B1C200000578-837_634x356 article-0-1B61B1CB00000578-444_634x356 article-0-1B61B1F500000578-922_634x352
Hata hivyo, Swala la kuingia katika Kanisa hili bila nguo limefanywa kuwa la hiyari hivyo kwa wale wanaojisikia kuingia wakiwa wamevaa nguo huendelea kufanya hivyo kama kawaida.



Love to hear what you think!