Saturday, September 21, 2013

PICHA NA JINSI TUKIO LA KUVAMIWA SUPER MARKET YA WESTGATE HUKO NAIROBI WESTLANDS


Kwa mujibu wa taarifa za sasa, takriban watu 20 wameripotiwa kuuawa na wengine 50 kujeruhiwa wakati ambapo mapambano ya bunduki yanaendelea kati ya polisi na watu hao wenye silaha walioiteka mall ya Westgate jijini Nairobi, Kenya.
article-2427892-1822C8DC00000578-605_638x365
Majeruhi wakisaidiwa kutoka kwenye eneo hilo
Shuhuda mmoja anadai aliwasikia watu hao wakiwaambia waislam wasimame na kuondokoa na kwamba wasio waislamu pekee ndio waliwalenga.
article-2427892-1822BC1B00000578-787_638x390
Majeruhi
Askari wa ulinzi walionekana wakitoa miili iliyotapakaa damu ikiwa imeweka kwenye matoroli ya supermarket.
_70036397_019379281-1
Huduma ya kwanza ikitolewa kwa majeruhi
Balozi wa Uholanzi nchini humo Rob Vandijk ameliambia shirika la AP kuwa alikuwa akipata chakula kwenye mgahawa uliomo ndani ya mall hiyo pindi watu hao wenye silaha waliporusha bomu hilo. Polisi wameizingira mall hiyo na harakati za kuwakomboa watu walioshikiliwa mateka kwenye mall hiyo zinaendelea.
article-2427892-1822C3CD00000578-409_638x397
Askari polisi akijiweka sawa
1Nairobi_2678725c
Ndugu wa baadhi ya watu walio ndani ya mall hiyo wakiwa na majonzi
Mall hiyo ni maarufu kwa kuwa na wateja wengi wenye kipato cha juu nchini humo na raia wa kigeni. Polisi imewataka wananchi wakae mbali na eneo hilo kwakuwa bado ni hatari.
article-2427892-1822BF2200000578-349_638x323
Polisi wakisaidia watu kutoka ndani ya mall hiyo
article-2427892-1822BF8200000578-325_638x377
Sababu za shambulio hilo hazijafahamika lakini vyombo vya habari nchini humo vinasema kundi hilo laweza kuwa magaidi ama majambazi walioenda kupora.
article-2427892-1822C0C100000578-913_638x584
article-2427892-1822C1E200000578-245_638x657
article-2427892-1822C59400000578-331_638x471
article-2427892-1822CB1C00000578-264_638x399



Love to hear what you think!