Friday, May 31, 2013

Photos: Afariki baada ya kuanguka akidandia daladala, Dar

afariki-akidandia-daladala-0

afariki-akidandia-daladala
Mtu mmoja ambaye jina lake bado halijafahamika, amefariki dunia baada ya kuteleza na kuanguka wakati alipokua akijaribu kudandia Daladala maeneo ya Ilala Boma, Jijini Dar es Salaam, asubuhi leo. Marehemu huyo baada ya kuanguka na kupiga kichwa kwenye lami, alipasuka kichwa na kuvuja damu nyingi kichwani, na kufariki katika eneo la tukio.


Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Amana, Ilala. Kwa habari na picha zaidi, nenda kwenye link ifuatayo:
Source: bongoclantz


Love to hear what you think!