Tuesday, March 19, 2013

PICHA 2 ZA NICKI MINAJ NA BIRDMAN WAKIINGIA HOSPITALI KUMSALIMIA LIL WYNE

.
Rapper Nicki Minaj wa Cash Money akiwasili kwenye hospitali alikolazwa Lil Wyne.
Uongozi wa lebo ya Cash Money yenye miliki ya vichwa kibao wakiwemo Nicki Minaj, Lil Wyne, Drake, Tyga, Busta na wengine.. umesema kuna upotoshwaji mkubwa juu ya taarifa za kuzidiwa kwa Lil Wyne ambae amelazwa hospitali toka wiki iliyopita huku media mbalimbali zikiripoti rapper huyo kuwa kwenye hali mbaya sana kiafya ambapo kalazwa kwenye  chumba cha wagonjwa mahututi.
Hata hivyo uongozi wa Cash Money umethibitisha kwamba mshkaji yuko salama na afya yake ni nzuri sasa hivi ndio maana imani yao ni kwamba atatoka hospitali very soon na kusisitiza kwamba taarifa za Wyne kuwa mahututi zilizosambaa mwanzoni zilikua za uongo.
Chanzo cha habari kilichokua kinatoa info kwa TMZ kimesema muda mfupi uliopita Lil Wyne ameonekana mwenye nafuu na hata kuweza kutembea humohumo ndani ya hospitali akiwa na walinzi wake.
.


Love to hear what you think!