Thursday, February 20, 2014

RAIS KIKWETE AELEZA MSIMAMO WAKE JUU YA HAKI ZA MASHOGA WALIOPO NCHINI TANZANIA

AKIHOJIWA  na CNN nchini Uingereza hivikaribuni wakati akihudhuria mkutano uliolenga kuongeza mapambano dhidi ya 
ujangili, Rais Jakaya Kikwete amepigilia msumari wa moto akisema Tanzania haiko tayari kukubaliana na matakwa ya baadhi ya nchi za magharibi zinazotaka nchi za Afrika ziwe na sheria zinazoruhusu ushoga.

"Itachukua muda kwa watu wetu kukubaliana na tamaduni za watu wa magharibi, nakumbuka Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron aliwahi kuzungumza sana kuhusu suala hilo na likaleta shida na tafrani kubwa kwa watu wetu," alisema.

"nafikiri kwa watu wetu sidhani kama huu ni muda muafaka wa kujadili suala hilo,hatulitaki na halikubaliki" alisema alipokuwa akihojiwa na mtangazaji wa CNN, Christiane Amanpour.

Amannpour alitaka kujua msimamo wa Rais Kikwete kuhusu haki za mashoga na harakati zinazofanywa ili kuufaya ushoga kama moja ya haki za msingi za binadamu



Love to hear what you think!