
Mwezi
wa pili walitofautiana baada ya bwana kuoa mke mwingine.Wakiwa
wametofautiana na Nasra kuendelea na maisha siku hiyo bwana akamfata
akamkuta barabarani anatoka kazini.Akiwa na rafiki yake wanatembea
akamfungia breki mguuni akamwambia anataka kuongea nae.Nasra akakataa
akamwambia kama kuna maongezi hawezi kuongea nae kama vipi amfate
nyumbani huku anaendelea kutembea.Bwana yule akamfata kwa nyuma
akamgonga na gari na baada ya Nasra kuanguka akanasa chini hivyo
kuendelea kumburuza umali wa kama mita 150 hivi.Alipofika kwenye tuta
akanasuka bwana ndio kushuka kwenye gari kukimbia.
Kiukweli aliumia sana sana ngozi yote ya mgongoni,mbavuni,makalio,ikavuka na kubaki kwenye lami.Sikio lake la kushoto lote likaliwa na lami,mbavu 7 zilivunjika pamoja na mguu.Akapelekwa hospitali na baadae kulazwa Bugando Mwanza lakini ikawa anahitajika kuhamishiwa hospital ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.Akiwa muhimbili alikuwa na hali mbaya sana baadae ikathibitika kuwa ameumia ndani kwa ndani kwani alibadilika sana akavimba na kuwa mweusi.Kwamuda wote wa miezi takribani sita alikuwa katika maumivu makali na bahati mbaya hakuweza kupambana tena kupigania maisha yake.
Nasra pichani kulia mwenye kilemba chekundu akiwa na ndugu zake wakati akiwa mzima.
Usiku wa kuamkia jumanne ya
tarehe 10 Nasra akaaga dunia.Ilikuwa ni huzuni sana jinsi alivyoteseka
na namna mazingira ya kifo chake kilivyotokea.Tulikuwa na matumaini kuwa
angeweza kupona maana dakika za mwisho alikuwa anaongea japo kwa shida.
Tunaomba mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Nasra mahala pema peponi,Amina.
SOURCE http://dinamarios.blogspot.com