Stori:Richard BukosiMALKIA
wa Muziki wa Taarab nchini anayelitumikia Kundi la Tanzania One Theatre
(TOT), Khadija Omary Kopa inadaiwa kuwa alianza kuona maruweruwe na
kukosa usingizi kabla ya kupewa taarifa za kifo cha mumewe ambaye ni
Diwani wa Kata ya Magomeni Wilayani Bagamoyo, Jafary Ally.

Kopa
aliyekuwa mkoani Rukwa na Kundi la TOT kwa ajili kutumbuiza kwenye
ziara ya Makamu wa Rais, Dokta Mohammed Ghalib Bilal, alikumbwa na
maruweruwe usiku kucha wakati mumewe akiteseka na kukata roho kwenye
Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Kwa
mujibu wa rafiki wa Kopa aliyekuwa Rukwa, usiku wa kifo cha mumewe,
malkia huyo alikosa usingizi na kukumbwa na maruweruwe mpaka walipopokea
taarifa za kifo cha mwanaume huyo.
“Niko naye jirani, hana nguvu za
kuweza kuzungumza lakini tupo Arusha tumeletwa na ndege ya makamu wa
rais, tunasubiri ndege nyingine ya kutupeleka Dar es Salaam na kuelekea
Bagamoyo kwa ajili ya mazishi,” alisema rafiki huyo wa Kopa.

Akizungumza
na gazeti hili, mama mzazi wa marehemu ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa
Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Tandale jijini Dar, Rehema Tuwa amesema
amepata pigo kubwa la kuondokewa na mwanaye tegemezi.

“Kinachoniuma
zaidi ni mwanangu kufariki dunia ghafla, Jumatatu tulimkimbiza
hospitali kutokana na homa kali, ghafla usiku wa kuamkia leo (juzi)
nashangaa kupewa taarifa za kifo, inaniuma sana,” alisema.